Skip to main content

MEYA MANISPAA YA IRINGA KIZIMBANI, WANA CHADEMA WENGINE WATANO WANYIMWA DHAMANA







MSTAHIKI Meya wa Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe (Chadema) amepandishwa kizimbani katika mahakama ya wilaya ya Iringa mapema leo akituhumiwa kutishia kumua kwa bastola, Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Manispaa ya Iringa, Alphonce Muyinga.


Pamoja na Kimbe, Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imewasomea mashtaka matatu wafuasi wengine watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) waliyofanya Novemba 19 wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kitwiru, Iringa mjini.


Wakati meya huyo ameachiwa kwa dhamana na mahakama ya wilaya Iringa baada ya kusota rumande kwa siku tatu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imewanyima dhamana wafuasi hao watano kwa kuwa kati ya makosa matatu wanayotuhumiwa kuyafanya kosa moja halidhaminiki.


Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Aristeck Mwinyikheri alisema Kimbe aliyefikishwa mahakamani hapo kwa kesi namba 189 ya mwaka 2017 anashitakiwa kutishia kumuua kwa Bastola Katibu huyo wa UVCCM kwa katika tukio lililotokea Novemba 26 mwaka huu katika kata ya Kitwiru, mjini Iringa wakati shughuli ya uchaguzi mdogo wa udiwani wa kata hiyo ikiendelea.


Mwinyikheri alisema meya huyo alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 89 (2) (a) cha kanuni za adhabu.


Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa John Mpitanjia alisema shauri hilo litarudi tena mahakamani hapo Desemba 12, mwaka huu wakati Meya huyo aliyedhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akikana kutenda kosa hilo.


Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa, wafuasi hao watano wa Chadema walioshitakiwa kupitia kesi namba 190 ya mwaka 2017 na kunyimwa dhamana ni pamoja na Martha Robert, Leonard Kulijira, Esau Bwire, Christopher Jevas na Samwel Nyanda.


Mbele ya hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Richard Kasele , mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo Chakila Felix alisema washitakiwa hao wanatuhumiwa kujeruhi, kuteka na kufanya unyang’anyi kwa kutumia nguvu.


Felix alisema watuhumiwa hao wanatuhumiwa kumjeruhi Dick Frank na kumnyang’anya simu yake ya mkononi.


Mahakama hiyo imewarudisha rumande kwa kuwa kosa la unyang’anyi kwa kutumia nguvu halina dhamana na shauri lao litarudi tena mahakamani hapo Desemba 12, mwaka huu. CREDIT: BONGOLEAKS

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...