Skip to main content

MIMBA ZA UTOTONI KUPUNGUA,SERIKALI YASHIRIKIANA NA MASHIRIKA BINAFSI KUTOA ELIMU,


Mkurugenzi Mtendaji wa Jukwaa la Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) Koshuma Mtengeti, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam


SERIKALI imejipanga kupunguza mimba za utotoni kwa asilimia 27 kwa kipindi cha miaka mitano kinachoanzia 2017 hadi 2022 lengo likiwa ni kuhakikisha mototo wa kike anapata haki yake ya elimu.


Hayo yamesema leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Maendeleo ya watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto, Margaret Mussai wakati wa Kongamano la Mtoto wa Kike , liloandaliwa na Jukwaa la Utu wa Mtoto wa Kike (CDF) kwa udhamini wa Shirika la Maendeleo Uswidi ( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA).


Mussai amesema kwa sasa serikali imeandaa mpango kazi wa Taifa wa kotokomeza ukatili wa kijinsi kwa upande Mimba za Utoto.


“Katika Mpango huu tumeanza kupunguza mimba kwa asilimia 27 kwa watoto na tunaamini mpango huu utasaidia kundokana na tatizo hili”amesema


Amesema katika kutekeleza mpango huu, Serikali itashirikiana Taasisi zisizo za Kiserikali katika kuhakikisha wanapunguza Mimba za Watoto.


Hata hivyo , Mussai amewataka Watoto wa Kike kujitambua wenyewe kwa kujiepesha na mambo yasio faa ambayo yatapelekea kuongezeka mimba za watoto ambapo amedai zimechangiwa na watoto hao kujiingiza kwenye makundi yasioa faa.


Kw upande wake Mkurugenzi wa Mtendaji wa CDF Koshuma Mtengeti, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwapatia fursa watoto wa kike kukurana na Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Uswid ambapo watapata fursa ya kuelezea mafunzo mbali mbali waliyopata kutokana na utekelezaji wa miradi mbali mbali ya CDF.


Amesema miradi hiyo ni pamoja na miradi ya kutokomeza, mimba za utotoni, ndoa za utotoni, ukatili wa kijinsia na kuonesha kazi za ujasiriamali walizozifanya ikiwa kama mafanikio ya miradi ya CDF.


“Vile vile katika kongamano hili, wanaume na wavulana wakiwa kama mabalozi wa CDF watapata fursa ya kuelezea ni kwa namna gani wanafanya kazi za kuelimisha jamii pamoja na vijana rika juu ya madhara ya ukatili wa kijinsia, ukeketaji, mimba za utotoni pamoja na ndoa za utotoni ili kufikia dhana ya Taifa ya kuleta usawa wa kiiinsia,” amesema Mtengeti.


Naye Mkurugenzi Mwandamizi kutoka SIDA Carin Jamtin, amesema shirika lao limekuwa likitetea haki za woto kwa kuhakikisha watoto wakike na kiume wanakuwa na haki sawa katika jamii hususani haki ya kupata elimu.


Mkurugenzi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo Uswidi ( Swedish International Development Cooperative Agency-SIDA) Carin Jamtin, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.


Mkurugenzi wa Maendeleo ya watoto kutoka Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii jinsia na Watoto, Margaret Mussai, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...