Skip to main content

RC AIPONGEZA RUAHA KWA KUPAMBANA NA UTAPIAMLO

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto) akitembelea banda la Ruaha Miling Company Limited katika uzinduzi wa Kampeni ya Mama Msosi Lishe mkoani Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)


Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza akimpatia uji wa lishe mtoto katika uzinduzi wa Kampeni ya Mama Msosi Lishe mkoani Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)



IRINGA: MKUU wa Mkoa wa Iringa (RC) Amina Masenza ameipongeza kampuni ya kusaga unga wa lishe ya ‘Ruaha Milling Company Limited’ ya mjini Iringa kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na tatizo la utapiamlo.

RC alisema huyo katika uzinduzi wa Kampeni ya Mama Msosi Lishe mkoani Iringa jana, ambayo ili lenga kuhamasisha lishe bora ili kupambana na udumavu pamoja na kuhamasisha usafi na uhifadhi wa mazingira.

Alisema kuwa kampuni ya Ruaha Milling imekuwa mstari wa mbele katika kupambana na utapiamlo mkaoni hapa kwa kutengeneza unga uliotiwa virutubisho.

Masenza alisema kuwa Kampeni ya Mama Msosi Lishe ni mojawapo ya njia ya kuboresha Lishe kwa familia na kuondoa matatizo yanayosababishwa na Lishe duni. 

“Wataalam wa masuala ya Lishe wanatuambia kuwa watoto waliopata huduma bora za Lishe, katika kipindi cha siku 1,000 za kwanza za uhai wao ambazo zinaanza tangu mama anapopata ujauzito hadi mtoto anapotimiza umri wa miaka miwili wanapata faida zitakazodumu katika maisha yao yote,” alisema.


Hiki ndicho kipindi mtoto anapojenga msingi wa ukuaji wa mwili na maendeleo ya akili. 

Kwa bahati mbaya madhara ayapatayo mtoto katika ukuaji wake kimwili na maendeleo ya kiakili kutokana na Lishe duni katika siku 1,000 za kwanza za maisha yake hayawezi kurekebishwa kwa maisha yake yote.

Kwa mujibu wa utafiti (TDHS, 2015/2016) umebaini kuwa hali ya Lishe ya wanawake na watoto bado ni mbaya Mkoani Iringa. 

Asilimia 28 ya wanawake wajawazito wana upungufu wa damu. Asilimia 42 ya watoto wamedumaa, asilimia 13.8 wana uzito pungufu, asilimia 3.6 wana ukondefu na asilimia 7.2 tu ndiyo wanalishwa vyakula vya nyongeza ipasavyo.

Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali umekuwa ukichukua hatua za kukabiliana na tatizo la utapiamlo. 

Hatua hizo ni pamoja na kutoa elimu ya Lishe katika vituo vya kutolea huduma, kutoa matibabu ya utapiamlo, kuhamasisha jamii kubadilli tabia za ulaji usiofaa na kufuata mtindo bora wa maisha, kuhamasisha usafi wa mazingira, kuwahi kliniki pindi mama anapogundua kuwa mjamzito. Na Friday Simbaya, Iringa

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...