Skip to main content

TASAF WILAYANI IRINGA WAPONGEZWA




Na Friday Simbaya, Iringa

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Andy Karas ameridhishwa na utekelezaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) wilayani Iringa kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini nchini kwa awamu ya tatu.

Karas alisema hayo jana walipotembea Kijiji cha Igingilanyi wilayani Iringa, mkoani Iringa na kujionea matokeo ya program mbalimbali zinazoendeshwa na USAID kama vile sekta ya kilomo, lishe, elimu,afya, wanawake na vijana na utawala bora.

Alisema kuwa amefurahishwa na hali za wanufaika kwa kuona baadhi ya wanufaika maisha yao yamebadilika kwa kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo ufagaji wa kuku na nguruwe.

“Nimefurahi sana kuona baadhi ya wananchi wakibadilika kimaisha kwa kuwa na makazi bora kupitia msaada unaotelewa na USAID kupitia mfuko wa maendeleo ya jamii kupitia mpango wake wa kunusuru kaya masikini,” alisema Karas.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Andy Karas alifanya ziara mkoani Iringa iliyoanza jumatatu hadi ijumaa wiki iliyopita kwa lenga la kujionea matokeo ya programu mbalimbali zinazoendeshwa na USAID mkoani humo pamoja na kufanya mazungumzo na wabia na walengwa wa programu hizo. 

Alisema kuwa ziara hiyo inaakisi wigo mpana wa miradi inayofadhiliwa na Marekani nchini Tanzania, ikijumuisha sekta za kilimo, lishe, elimu, afya, wanawake na vijana na utawala bora.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Miradi wa TASAF, Amadeus Kamagenge amelipngeza Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) katika kusaidia juhudi za serikali za kuwaondoa wananchi wanaokabiliwa na umasikini. 

“TASAF ni mpango wa kunusuru Kaya maskini na imekuwa katika awamu tatu mpaka hadi sasa kwa ajili ya kuwezesha Kaya maskini kujikwamua kiuchumi,” alisema Kamagenge.

Jumla ya kaya 97 za Kijiji cha Igingilanyi zinanufaika na mfuko wa maendeleo wa jamii kupitia mpango wa kunusuru kaya masikini ambapo imeelezwa kuwa kaya hizo zimelipwa mara 14 na zaidi ya milioni 49 zimetolewa kwa wanufaika.


Hata hivyo, serikali imejipanga kuborsha zaidi mpango wa kunusuru Kaya masikini nchini ujulikanao kama TASAF kwa awamu ya tatu kwa kutengeneza miundombinu mizuri ya kutambua Kaya zinazolengwa na kuondoa malalamiko ya wananchi kuwa mpango huu umekuwa ni wa Kaya chache na fedha hizo utolewa kwa upendeleo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...