Skip to main content

DKT MWANJELWA AIAMURU TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO MTWARA KUWAONGEZA MALIPO...


Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua miche ya Korosho wakati alipotembelea Kitalu Nyumba (Green House) katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara Mwingine ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Dkt Omari Mponda, leo 22 Disemba 2017. Picha Zote Na Mathias Canal

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua Tanki linalohifadhi maji kwa ajili ya Skimu ya umwagiliaji wakati alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara, leo 22 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akishiriki kazi ya kubangua korosho wakati alipotembelea Kiwanda cha Korosho na Juice katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwara, leo 22 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua shamba lenye mfumo wa kisasa wa umwagiliaji kwa Skimu ya umwagiliaji wakati alipotembelea Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara, leo 22 Disemba 2017.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua miche ya Korosho wakati alipotembelea Kitalu Nyumba (Green House) katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Mkoani Mtwara Mwingine ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) Dkt Omari Mponda, leo 22 Disemba 2017. 
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akishiriki kazi ya kubangua korosho wakati alipotembelea Kiwanda cha Korosho na Juice katika Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) wakati wa ziara yake ya kikazi Mkoani Mtwara, leo 22 Disemba 2017.


Na Mathias Canal, Mtwara


Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele (NARI) ambayo Kitaifa inaratibu Utafiti wa zao la Korosho, Mbegu za mafuta na mazao jamii ya mizizi (Muhogo na viazi vitamu) Dkt Omari Mponda ameagizwa kuwaongeza malipo ya kazi wafanyakazi wa kituo hicho katika mradi wa kubangua Korosho.


Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa leo 22 Disemba 2017 wakati akizungumza na wafanyakazi wa kituo hicho cha Utafiti Mara baada ya kutembelea kiwanda kidogo cha kubangua Korosho na kubaini kuwa wafanyakazi hao wanalipwa shilingi 600 kwa kila kilo moja ya korosho wanayobangua kiasi ambacho hakiakisi ufanisi wa kazi kubwa wanayoifanya.


Katika maelekezo yake Naibu Waziri huyo amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa kituo hicho kuongeza kiasi cha malipo walau kufikia shilingi 1000 kwa kila kilo moja wanayobangua ili wafanyakazi hao waweze kupata malipo ambayo yatamudu gharama za maisha.


Sambamba na hayo pia ameupongeza Uongozi wa kiwanda hicho kwa kubuni ajira hizo mpya za mradi huo wa korosho zinazowanufaisha wananchi wa Mtwara sambamba na pongezi za kuajiri wafanyakazi wengi ambao asilimia kubwa ni wanawake.


Aidha, amesisitiza kuongeza bidii ya utoaji Elimu kwa wananchi kufahamu umuhimu wa mazao ya muhogo, Njugu na Mbaazi ili yaweze kutumika zaidi kwani ni fahari kwa wakulima na wananchi kwa ujumla.


Katika hatua nyingine Mhe Mwanjelwa ameipongeza Taasisi hiyo kwa kufanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza Afrika kutoa/kugundua na kusajili mbegu bora 54 za korosho kwa ajili ya matumizi kwa wakulima mwaka 2006 (Aina 16), Mwaka 2015 (Aina 22 mbegu chotara), na Mwaka 2016 (Aina 16 mbegu fupi).


Alisema Aina hizo za mbegu hizo zina uwezo wa kuzaa korosho nyingi na bora, Zina uwezo wa kuvumilia magonjwa na wadudu waharibifu na kufanya Utafiti kupendekeza zaidi ya Aina 30 za viuatilifu vya kudhibiti visumbufu vya Korosho.


Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele (NARI) imepewa jukumu la kufanya Utafiti ili kuongeza tija katika Kilimo katika kanda ya kusini mikoa ya Lindi, Mtwara na Wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma.


MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...