Skip to main content

SHILINGI MILIONI 100 ZAKOPESHWA KWA WANAWAKE NA VIJANA MUFINDI

Sehemu ya Viongozi wa Makundi 37 ya Wanawake na Vijana wakiwa ndani ya ukumbi wa Halmashauri kupokea hundi za Vikundi vyao.


Viongozi katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Vikundi wakiwa wameshika hundi zilizoambatishwa na Vocha.


Jumla ya s
hilingi Milioni 100, zimetolewa kwa sharti la Mkopo kwa vikundi vya Wanawake na Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, ikiwa ni utekelezaji wa takwa la sheria inayozitaka mamlaka za Serikali za mitaa nchini kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa lengo la kuwakopesha vijana na Wanawake ili wajiajiri kupitia shughuli za kijasirimali hivyo kuboresha maisha yao.

Akisoma taarifa ya Mikopo hiyo, Mkuu wa Idara ya maendeleo ya jamii Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Bw. Hatibu Bwashehe, ametanabaisha kuwa, kati ya vikundi hivyo, vikundi 22 vya wanawake vimekopeshwa jumla ya shilingi Milioni 62, wakati vikundi 15 vya Vijana vimenufaika na Mkopo huo kwa kupata shilingi Milioni 38.

Akizungumza kabla ya kukabidhi hundi kwa walengwa, mgeni wa heshima katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Mh. Jamhuri William, amevitaka vikundi hivyo vielewe kuwa, fedha wanazopokea ni Mkopo hivyo, zitumike kulingana na maandiko waliyowasilisha badala ya kuzitumia kwa malengo tofauti kama vile kuchangia harusi au kununua mavazi ya kifahari na kuongeza kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa kutorejesha fedha za Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Mh. Festo Ngina, amepongeza mwenendo mzuri ya urejeshaji Mikopo kwa vikundi vilivyokopeshwa kiasi cha shilingi Milioni 300 kwa mwaka wa fedha uliopita wa 2016 – 2017 na akaongeza kuwa ili hali ya urejeshaji izidi kuwa bora zaidi, Watendaji wa kata na Vijiji watahusika kufuatilia marejesho hayo kama ambavyo wanahusishwa kwenye chakato kusajili vikundi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mtendaji wa wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Profesa Riziki Shemdoe, amewahimiza Vijana na Wanawake wa Halmashauri hiyo kuendelea kuwasilisha maombi kwa kuwa Halmashauri yake tayari imetenga fedha nyingine kiasi cha shilingi Milioni 140 ambazo watazikopesha baadaye mwezi ujao mara baada ya kukamilisha uchambuzi wa maandiko ambayo yatakuwa yanalenga kuanzisha viwanda Vidogo.

Aidha, wanufaika wa Mkopo huo ambao ni Wanawake na Vijana, wameipongeza Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais John Pombe Magufuli, kwa kuwathamini na kuwapatia mikopo hiyo huku wakiahidi kuzitumia kwa malengo na kurejesha kwa wakati.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...