Skip to main content

SIDO YATOA MKOPO WA KILIMO KWA KIKUNDI CHA UPENDO WILAYANI KILOLO


Ofisa Biashara wa Sido Niko Mahinya


Ofisa Mikopo wa SIDO Mkoa wa Iringa Neserian Laizer



KILOLO: SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogovidogo (SIDO) Mkoa wa Iringa katika kuunga juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kupambana na wimbi la umasikini limekikopesha kikundi cha Upendo IR Vicoba cha Kijiji cha Mtandika kiasi cha shilingi milioni kumi na tatu na laki tatu (13.3m/-) kwa ajili ya kuweza kuwasaidia kuendesha shughuli za kilimo. 

Akizungumza na viongozi na wajumbe wa kikundi hicho cha wakulima kilichopo wilayani Kilolo, katika hafla fupi ya kukabidhi cheki ya fedha iliyofanyika katika Kijiji cha Mtandika, Kata ya Ruaha-Mbuyuni, Ofisa Mikopo wa SIDO Mkoa wa Iringa Neserian Laizer alisema kuwa wamekikopesha kikundi cha wakulima ili kuwainua kiuchumi na kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo. 

Ofisa mikopo huyo alisema kwamba wamebaini katika maeneo mengi ya vijiji kuna fursa nyingi zilizopo katika zao la kitunguu lakini baadhi ya wakulima wanashindwa kutimiza malengo yao waliyojiwekea kutokana na kukosa mtaji wa fedha. 

“ …hivyo wakiwezeshwa wataweza kutumia fursa zilizopo za kilimo kwenye maeneo yao ili kuleta mabadiliko chanya ya kukuza uchumi,” alisema Laizer. 

Naye Ofisa Biashara wa Sido Niko Mahinya aliongeza kuwa Shirika hilo lengo lake kubwa ni kuwasaidia fedha za mitaji wakulima ili waweze kujiendeleza zaidi sambamba na kuwajengea uwezo wa wakuzalisha kitunguu katika ubora unaotakiwa pamoja kuwatafutia masoko. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikundi cha wakulima cha Upendo IR Vicoba kilichopo katika kijiji cha Mtandika Salama Maulidi Chowanga alilipongeza shirika la Sido kwa kuwapatia mkopo huo licha ya kukabiliwa na changamoto ya soko la zao la kitunguu. 

Mwenyekiti huyo alisema kwamba wanakundi ambao wamepatiwa mikopo wanaitumia kwa malengo yaliyokusudiwa pamoja na kuhakikisha wanachama wanarejesha mkopo kwa wakati. 

Naye katibu wa kikundi Zamoyoni Zigo alisema kuwa kikundi cha kinajumla ya wanachama 30 lakini waliopatiwa mikopo ni wanachama 29, mmoja walikosa mkopo kutokana na matatizo ya kifamilia. 

Mwsho 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...