Skip to main content

DKT KIGWANGALLA ASITISHA VIBALI VYA KUHAULISHA MISITU YA HIFADHI ....



Waziri wa maliasli na utalii dkt hamisi kigwangalla akiongoza kamati ya misitu kutembelea msitu wa hifadhi wa Kihesa kilolo uliopo manispaa ya IRINGA kujiridhisha na mipaka kabla ya kuhaulisha sehemu ya msitu huo wenye ukubwa wa zaidi akari 500 kwa ajili shughuli za utalii jana. (Picha na Friday Simbaya)

Image may contain: plant, tree, outdoor and nature

WAZIRI wa maliasili na utalii Dk.Hamis Kigwangala amewaagiza wakuu wa mikoa kote nchini kwamba wasihangaike kuandika barua za kuomba kuhaulisha misitu ya vijiji au halmashauri ili zitumika kwa shughuli za maendeleo.

“Mimi hapa, nina msimamo mkali sana,Naomba Taifa lifahamu, lijuwe na viongozi wote wafahamu wasithubutu kuleta maombi ya kuhaulisha misitu iliyohifadhiwa kwa sababu hayo maombi nimekwisha yakataa kabla hayajafika mezani kwangu.”amesema Dk. Kigwangala na kuongeza: 

“Kwa kipindi ambacho nitakuwa waziri wa mali asili na utalii sitohaulisha misitu hivyo viongozi wasahau kupoteza muda wao kuomba maeneo yaliyohifadhiwa kwamba yahaulishwe kwa ajili ya makazi,kilimo au shughuli nyingine za maendeleo hilo halitofanyika wakati mimi nikiwa waziri.”alisema Dk.Kigwangala

Dk.Kigwangala amesema hayo jana kwenye mkutano wa tatu wa kamati ya kitaifa ya ushauri wa misitu (National Forestry Advisory Committee -NAFAC) uliofanyika mjini Iringa.

Kamati hiyo ilifika mjini Iringa kwa lengo kupitia mapendezo ya kuhaulisha sehemu ya msitu wa Kihesa kilolo uliopo katika manispaa ya Iringa ambapo manispaa iliomba eneo hilo litumike kwa ajili ya shughuli za utalii.

Pia kamati hiyo ilifika kufuatia mapendekezo aliyoyowasilishwa katika kikao cha pili cha kamati ya mwaka jana kama eneo waliloomba ni sahihi ama la.

Dk.Kigwangala alisema kuwa amekuwa na ndoto ya kutaka kubadilisha misitu iliyokuwa ikisimamiwa na kundeshwa na vijiji au halmashauri kumilikiwa na serikali.

“Katika mambo ambayo mimi sikubaliani nayo ni kwamba kuna misitu zipo kwenye halmashauri na vijiji lakini ruhusa ya kutumia inatoka serikalini hii ni mambo ambayo sikubali kwa sababu misitu inapotea,inateketea na umiliki na uendeshaji wa misitu kwa mamlaka za chini zimeonekana hazina faida zozote kwenye uhifadhi hivyo ni wazo ni ndoto nimekuwa nayo baada ya kujifunza namna wizara ya mali asili inatekeleza majukumu yake na nikaona hapa kuna mapungufu makubwa.”alisema Dk.Kigwangala.

Katika hatua nyingine amesikitishwa kuona sekta ya misitu nchini ikichangia pato dogo la taifa ambapo takwimu zinaonesha misitu inachangia takribani asilimia 3.7 katika pato la taifa.

“Sisi kama wizara haturidhishi na mchango huu bado tunaona upo chini sana kiasi cha kutishia kutoaminika kwa takwimu hizi,hili ni eneo ambalo tunaona nilakufanyia kazi iwezekanavyo na hivyo ninaomba kamati hii ije na ushauri ni kwa jinsi gani tunaweza kutumia sekta hii katika kuongeza pato la taifa.”alisema Kigwangala.

Hata hivyo aliomba kamati ya ushauri ya misitu kuja na ushauri wa jinsi gani wanaweza kuitumia sekta huyo ya misitu katika kuongeza mchango wake katika pato la taifa.

“Kama wizara tunataka tulitazame kwa upya eneo hili la matumizi ya mkaa kama nishati pekee inayotumiwa na wananchi wingi katika kupikia na kuona ni kwa jinsi gani tunaweza tukalitumia zao hili vyema ili kuongeza mapato.” alisema Dk. Kigwangala.

Naye naibu waziri wa mali asili na utalii Japheth Hasunga alisema kuwa alimpongeza mkuu wa mkoa huo kuhakikisha korido ya kusini inafunguka kwenye sekta ya utalii.

“Katika kipindi cha mwaka 2017 watu wengi walienda kutembelea hifadhi za ndani,utalii wa nchi hii unatakiwa utokane na utalii wa ndani wale wa nje iwe ni nyongeza.”alisema Hasunga nakuongeza:

“Najuwa kamati hii itakushauri mambo mengi katika masuala mazima ya misitu kwa ajili ya maendeleo ya nchi hii na vizazi vijavyo lakini pia tunategemea sana katika kutoa mwelekeo wa namna bora wa kutumia rasilimali hii na kuhakikisha inazalisha faida.”alisema Hasunga.
Image may contain: 1 person, sitting, table and indoor
Katika kipindi kifupi wameshughudia mambo mengi yametokea katika hifadhi ikiwamo malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusiana na hatua mbalimbali ambazo serikali inachukua katika kuhakikisha usimamizi wa mali asili hizo zinakuwa mathubuti.

“Huenda tunafanya sawa au tunakosea hivyo kazi ya kamati hii ni kutushauri sisi kama tunachokifanya sawa au sio sawa huku akiwataka wajumbe hao kufanya kazi yao kwa weledi na kwa kuzingatia taaluma waliyo nayo.”alisema Hasunga.

Naye mkuu wa mkoa huo Amina Masenza aliomba wizara hiyo kufikiria ombi lao la kutaka kuhaulisha sehemu yam situ huo ili waweze kufanya shughuli za utalii huku akihaidi kufanyia kazi maagizo ya wizara ikiwamo kuondoa dampo kwenye eneo la msitu uliohifadhiwa,kuweka mipaka.

Kamati hiyo iliambatana na Waziri wa mali asili na utalii Dk.Hamis Kigwangala,Naibu waziri wa wizara hiyo Japhet Hasunga,Naibu katibu mkuu wa wizara hiyo Dk.Aloyce Nzuki pamoja viongozi wa mkoa wa Iringa kutembelea msitu huo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...