Skip to main content

MADIWANI WANNE WAPYA WAPISHWA MANISPAA YA IRINGA



Diwani wa Kata ya Kitwiru (kushoto)kupitia CCM anakula kiapo mbele ya Baraza la Madiwani la Manispaa ya Iringa katika Jimbo la Iringa Mjini huku hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa David Ngunyale (kulia) akisimamia kiapo hicho jana. (Picha na Friday Simbaya)




Diwani wa Viti Maalum Rehema Mbetwa (kushoto) anakula kiapo mbele ya Baraza la Madiwani la Manispaa ya Iringa huku hakimu mfawidhi wa mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa David Ngunyale (kulia) akisimamia kiapo hicho jana. (Picha na Friday Simbaya)



MADIWANI wanne wapya wa Manispaa ya Iringa wawili kutoka CCM na wawili kutoka Chadema wameapishwa leo na kukabidhiwa nyaraka mbalimbali tayari kwa kuanza kazi ya uwakilishi wa wananchi katika maeneo yao jana. 


Walioapishwa katika baraza la madiwani ya robo ya pili ya mwaka 2018 ni pamoja na Jully Sawani kupitia CCM kata ya Kihesa ambaye katika uchaguzi wa Janauri 13 alipita bila kupingwa baada ya vyama vya upinzani kususia uchaguzi. 


Mwingine ni aliyewahi kuwa diwani wa kata ya Kitwiru Baraka Kimata ambaye Agost mwaka jana alijiuzuluwa wadhifa wake wa udiwani wa kata ya Kitwiru na kujiunga na CCM ambapo katika uchaguzi wa Novemba 26 alichaguliwa tena kuwa diwani wa kata ileile kupitia CCM. 


Madiwani wengine wawili ni waviti maalum amabo ni Maimuna Mpogole na Rehema Mbetwa wote wa Chadema, wawili hao wameteuliwa na tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC kuziba nafasi iliyoachwa wazi na Leah Mleleu na Husna Daudi ambao walitimika Chadema na kuhamia CCM. 


Akizungumza mara baada ya kuapishwa kwa madiwani hao Meya wa Manispaa ya Iringa Alex Kimbe amewataka madiwani hao kusoma vizuri kanuni za uendeshaji wa baraza la madiwani ili waweze kuwa na mchango chanya kwenye halmashauri yao. 


naye Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela ambaye alihudhuria kikoa cha baraza hilo la madiwani kama mshauri wa baraza hilo aliwapongeza madiwani wote walioapishwa, lakini akawaomba wakazi wa Iringa kuacha siasa za chuki alizodai kwamba hazina tija kwao na kwa taifa lao. 


Alisema vyama visiwagawe wananchi na kwamba si jambo jema kutendeana vitendo vibaya kwa kuwa hata mbinguni hakuna vyama vya siasa. 


Maidwani walioapishwa wamedai wamejipanga kuzitumikia nyazifa zao walizopatiwa na wananchi kwamba watahakikisha wanakuwa na uwakilishi chanya kwenye halmashauri yao. 


"Mimi kwanza ni washukuru wananchi walionichagua, nilikuwa diwani na nimeapishwa kuwa diwani tena safari hii ni kitokea Chama kinachoshikilia dola na ambacho ilani yake ndiyo inayotekelezwa,"alisema Baraka Kimata diwani kata ya Kitwiru. 


Diwani wa kata ya Kihesa Jully Sawani alisema yeye amejipanga kufanya kazi na asingependa kuwa mtu wa maneno maneno. 


"Mimi niwaombe wakazi wa kata ya Kihesa ushirikiano, tuachane na mambo ya siasa tufanye kazi za maendeleo, tuachane na siasa, siasa hizi za vyama zisitutangenishe sisi,"alisema Sawani. 


Madiwani wote wa viti maalumu walisema wao wanashukuru chama chao na uongozi wa Halmashauri kwa kuwaamini na kuwafanya kuwa sehemu ya baraza la madiwani na kwamba watahakikisha wanawajibika ipasavyo. 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...