Skip to main content

Mama Samia aahidi kupunguza msongamano hospitali ya Mafinga








Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amesema serikali imeanza kupanua vituo vya afya nchini pamoja na kuboresha huduma za matibabu ili kupunguza msongamano wa watu katika hospitali za wilaya. 

Mama Samia alitoa kauli hiyo hivi karibuni alipotembelea na kuweka jiwe la msingi na kukagua maendeleo ya upanuzi wa Kituo cha Afya Ihongole katika Kijiji cha Ihongole nje kidogo ya Mji wa Mafinga, wilayani Mufindi mkoani Iringa. 

Alisema kuwa Serikali itaendelea kutoa kipaumbele katika boresha utoaji wa huduma afya katika vituo vya afya katika wilaya ili kupunguza msongamano mkubwa uliopo kwenye hospitali za wilaya pamoja nza mikoa. 

“Tukishapunguza msongamano madaktari wetu watafanya kazi kwa uhakika zaidi na kwa umakini mkubwa,” aliongeza makamu wa rais. 

Hata hivyo, makamu wa rais halmashauri ya mji wa mafinga, wilayani Mufindi kwa kutumia fedha vizuri zilizotoalewa na serikali kwa ajili ya shughuli za upanuzi wa kituo cha Ihongole. 

Awali akitoa taarifa ya mradi wa upanuzi wa kituo cha afya Ihongole, Mkugurenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga Saada Mwaluka, alisema Kituo cha Afya Ihongole kilianza kutoa huduma mwaka 2008 ambapo kilikuwa kinahudumia wastani wa watu 5,000 kwa mwaka. 

Kwa sasa kinahudumia wastani wa watu 26,032 kwa mwaka ikiwa ni ongezeko la wastani wa watu 21,032 kutoka katika kata ya Boma na kata jirani za Kinyanambo, Changarawe na Isalavanu. Mradi wa upanuzi wa Kituo ulianza mwezi Novemba 2017. 

Alisema kuwa Mradi huu ni juhudi za Serikali katika kuhakikisha inasogeza huduma za Afya kwa wananchi yanafikiwa. 

Mawluka alisema kuwa lengo la mradi huo ni kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kwa kuimarisha Miundombinu katika kituo ili kiweze kutoa huduma za upasuaji wa dharura na huduma ya kuongeza damu. 

Alisema kuwa ili kufanikisha hilo, mradi umelenga kuongeza majengo ya Upasuaji, Maabara, wodi ya Wazazi, nyumba ya Mtumishi na kuhifadhia Maiti pamoja na kufanya ukarabati wa majengo ya zamani. 

Mwaluka alisema upanuzi wa majengo ya kituo cha afya pia utasaidia kuboresha utoaji wa matibabu katika kituo hicho cha Ihongole na hatimaye kupunguza msongamano wa hospitali ya wilaya Mafinga. 

Alisema kuwa Ujenzi na ukarabati wa kituo hiki cha Afya, unaotarajiwa kukamilika wakati wowote kuanzia sasa, baada ya serikali kutoa kiasi cha Shilingi Milioni saba na ishirini (720) kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya kituo hicho ili kiweze kukidhi haja ya kutoa huduma bora za Afya kwa zaidi ya Wananchi. 

Mwaluka alisema ujenzi na ukarabati wa kituo, utatekelezwa kwa mfumo wa (Force Account) ambapo, Halmashauri itatumia Mafundi wenyeji watakaothibitishwa kuwa na uwezo unaokubalika wa kutekeleza jukumu hilo. 

Halmashauri ya Mji Mafinga ina jumla ya wakazi 71,641 kati yao wanaume ni 34,522 na wanawake 37,119 (Sensa ya watu na makazi 2012). 

Halmashauri ina jumla ya vituo 21 vya kutolea huduma za Afya, ikiwemo Hospitali 1, vituo vya Afya 5 (2 vya serikli na 3 visivyo vya Serikali) na zahanati 15 (9 za 
serikali na 6 zisizo za Serikali). 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...