Skip to main content

MEYA MANISPAA YA IRINGA ABADILISHIWA HATI YA MASHITAKA

 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Iringa imeahirisha kesi inayomkabili Meya wa Maanispaa ya Iringa Alex Kimbe ya kutishia kuua mtu kwa bastola hadi kesho baada ya mwendesha mashitaka wa upande wa Jamhuri kubadilisha hati ya mashitaka ya kesi hiyo. 


Kesi hiyo namba 189 ya mwaka 2017,ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa hoja za awali na upande wa Jamuhuri ulidai uko tayari lakini wakili wa upande wa utetezi Samson Rutebuka alidai mahakamani hapo kuwa hakuwa tayari kwa hatua hiyo kutokana na kuhitaji muda kwa ajili ya kujisoma kabla ya kuanza usikilizwaji wa kesi hiyo.

Hakimu Mpitanjia alihoji upande wa Jamuhuri sababu za wakili wa utetezi kutopatiwa hati hiyo hadi jana ambapo alijibiwa kuwa ni kutokana na dhamira ya Jamhuri kutaka kubadilisha hati ya Mashitaka.

"Mheshimiwa Hakimu tumeshindwa kumpatia wakili wa utetezi hati ya mashitaka kwa kuwa tunatarajia kuwasilisha ombi la kubadilisha hati hiyo ,hivyo tusingempatia kabla haijasajiliwa mahakamani,'alisema Mwita.

Hakimu alikubaliana na ombi la upande wa Jamhuri na kuruhusu hati hiyo isomwe upya huku pia akikubaliana na upande wa utetezi wa kuahirisha kesi hiyo hadi kesho itakapoanza usikilizwaji wa hoja za awali.

Katika hati hiyo iliyosomwa jana na Wakili wa serikali Mwita, mahakama ilielezwa kuwa mtuhumiwa anashitakiwa kwa makosa mawili la kwanza ni la kukutwa na risasi nyingi kuliko kibali chake kinyume na kifungu namba 22 (1) a na 60 (1) cha umiliki wa siraha ya mwaka 2015.

Ilidaiwa kuwa mnamo Novemba 26 mwaka jana katika eneo la Zizi ndani ya wilaya ya Iringa mtuhumiwa alikutwa na risasi nyingi kinyume na sheria.

Katika kosa la pili ilidaiwa kuwa Novemba 26 mwaka jana katika eneo la kata ya Kitwiru wilaya ya Iringa mtuhumiwa alitishia kumuia Alfonce Patrick kinyume na sheria kifungu cha 89(2) (a ) cha Kanuni ya adhabu.

Mtuhumiwa alikana makosa yote mawili na kesi hiyo inatarajia kuaendelea kesho mahakamani hapo kwa usikilizwaji wa hoja za awali baada ya upande wa mashtaka kudai umekamilisha upelelezi.

Kimbe alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza Novemba 28, kabla ya kuahirishwa hadi Desemba 12, mwaka jana kisha kupangiwa Januari 11 mwaka huu aliahirishwa hadi Januari 29 na kisha kupangiwa February 5. 

Kesi hiyo inatarajia kuaendelea leo kwa kuanza usikilizwaji wa hoja za awali baada ya upande wa mashitaka kudai uko tayari kwa hatua hiyo na upande wa utetezi ukidai utakuwa umekamilisha zoezi la kupitia nyaraka za kesi husika. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...