Skip to main content

MKUU WA WILAYA AWAAMURU MADEREVA KUSHUSHA MBOLEA



Mkuu wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Luckness Amlima Leo ameamuru mbolea iliyokuwa imeletwa wilayani humo kwa ajili ya wakulima wa zao la Tumbaku na madereva kuzuia kushusha mbolea hiyo wakidai walipwe gharama za usafirishaji wa mbolea hizo ameamuru zishushwe mara moja na wagawiwe wakulima.

Akiongea na madereva na wakulima hao katika viwanja vya ushirika wilayani humo mkuu wa wilaya huyo alisema kuwa hakuna sababu ya kuendelea kubaki na mbolea kwenye magari huku wakulima wakilalamikia tumbaku inaharibika kwa kukosa mbolea.

“Shusheni mbolea kwani madai ya fedha ya kusafirishia mbolea hiyo yanafanyiwa kazi na chama kikuu cha Ushirika SONAMCU alisema mkuu wa wilaya huyo.

Aidha mwandishi msaidizi wa chama cha msingi Namtumbo bwana Nasoro Makomaye alisema kuwa mbolea ilifika wiki mbili zilizopita lakini madereva walikataa kushusha mbolea hiyo wakidai fedha ya kusafirishia mbolea hiyo.

Bwana Nasoro alimshukuru mkuu wa wilaya ya Namtumbo kwa kuwasikiliza kilio chao cha kushusha mbolea hiyo na wakulima wagawiwe mbolea hiyo na waweze kuitumia katika zao la Tumbaku.

Hata hivyo bwana Nasoro aliongeza kuwa kitendo cha mbolea hiyo kucheleweshwa itasababisha mapato ya uzalishaji wa zao la tumbaku kushuka na hasa ukizingatia muda wa kuweka mbolea kwenye zao hilo ulisha pita.

Naye Hamisi Rajabu Lyemo mkulima wa zao la Tumbaku alidai kuwa pamoja na mkuu wa wilaya kuwasaidia katika kuhakikisha mbolea hiyo inateremshwa na wanagawiwa wakulima bado mbolea hiyo haina tija sana kwa wakulima kutokana na namna ilivyochelewa kuletwa kwa wakati.

Bwana Hamisi alidai alipamba tumbaku shambani kwake tarehe 11.Desemba mwaka huu na alitakiwa kuweka mbolea siku saba baada ya kupanda yaani tarehe 18Desemba lakini tumbaku hizo zimekomaa bila mbolea na kuonesha wasiwasi wake katika uzalishaji wa zao hilo pamoja na kukosekana kwa ubora wa zao hilo.

Madereva wa magari yaliyoamriwa kushusha mbolea hiyo bwana Elieza Mshana na Hamza Shelukindo wakazi wa Dar-es-salaam walidai wanakubaliana na maamuzi ya mkuu wa wilaya kushusha mbolea na kumwomba mkuu wa wilaya huyo kusimamia malipo yao ya usafirishaji wa mbolea hiyo .

Katibu wa mbunge wa jimbo la Namtumbo Kalela Amimu ambaye ndiye msimamizi wa ugawaji wa mbolea hizo alisema kuwa mahitaji ya mbolea katika wilaya ya Namtumbo ni mifuko 11061 ikiwa mbolea ya NPK ni mifuko 6,617 mbolea ya CAN mifuko 2,222 na mifuko 2,222 ya UREA ambapo mpaka sasa mbolea iliyopokelewa ni mifuko 6000 pekee.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...