Skip to main content

RC Masenza Awataka Wakandarasi Kufanya Kazi Kwa Ufanisi Na Viwango Vya Ubora







Mratibu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Iringa Iringa Eng Juma Wambura (wa pili kulia) akimkabidhi mmoja wakandarasi mkataba (Picha na Friday Simbaya)







IRINGA: Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amewataka wakandarasi wote walioshinda zabuni kufanya kazi kwa kuzingatia muda uliopangwa na viwango vya ubora wa kazi. 

Alisema kuwa Serikali haitamvumilia mkandarasi yeyote atakayefanya kazi chini ya muda uliopangwa kwenye Mkataba, Lakini pia haitamvumilia Mkandarasi atakayefanya kazi chini ya viwango. 

RC Masenza alisema hayo jana wakati akishuhudia hafla fupi ya kutiliana saini mikataba ya miradi ya ujenzi wa barabara kati ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Iringa na wakandarasi walioshinda zabuni kwa mwaka wa fedha 2017/2018. 

Alisema kuwa katika kuhakikisha ufanisi wa kazi na ubora unaotakiwa, Serikali imeajiri Mameneja wa TARURA katika kila halmashauri. 

“Jukumu kubwa la Mameneja hawa ni kuwasimamia wakandarasi ili watekeleze wajibu wao. Hivyo, Mameneja wa Halmashauri pia mjipange sawasawa kuhakikisha ubora na thamani ya fedha inapatikana,” alisema. 

Alisema kuwa kumekuwa na changamoto ya malipo kwa wakandarasi na changamoto nyingi zimekuwa zikisababishwa na uzembe na kutokufuata taratibu. 

Masenza alisema anamatumaini kuwa wakandarasi hawa watalipwa kwa wakati baada ya kuwa wametimiza wajibu wao, wamefikia vigezo vya ubora kwa mujibu wa mikataba, na kuongeza kuwa utekelezaji huo utawafanya kuongeza morari ya kazi na pia kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima kwa Serikali. 

“Namuagiza Mratibu wa TARURA Mkoa kusimamia na kuratibu shughuli zote za ujenzi na ukarabati ikiwa ni pamoja na kuwasimamia Mameneja wa TARURA wa Halmashauri kutekeleza majukumu yao na Wakandarasi kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Mikataba,” alisema. 

Lakini pia alimtaka Mratibu wa TARURA Mkoa kuweka utaratibu mzuri utakaowaripoti Wakandarasi watakaoshindwa kwenda na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya Rais, Dr. John Magufuli na watakaofanya kazi kwa kulipua ili taarifa zao ziwasilishwe kwa mamlaka husika na hatimaye waweze kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria za nchi na ikiwezekana wasipewe tena kazi za ujenzi. 

“Nichukue nafasi hii tena kuwapongeza wakandarasi walioshinda zabuni za ujenzi na kusaini mikataba ya ujenzi wa barabara kwa mwaka wa fedha 2017/2018 katika mkoa wa Iringa. Natumaini uzalendo kwa nchi utawekwa mbele kwa maslahi mapana ya Tanzania na maendeleo ya nchi yetu,” alisema RC Masenza. 

Kwa upande wake, Mratibu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Iringa Iringa Eng Juma Wambura alisema kuwa mikataba kati ya wakandarasi walioshinda zabuni na TARURA ya Miradi ya Barabara kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ni kuwa gharama ya shilingi za kitanzania bilioni 3.56. 

Eng. Wambura alisema kuwa TARURA imechukua majukumu ya kiutendaji kuhusiana na ujenzi na matengenezo ya mtandao wa barabara za vijijini na mijini ambayo yalikuwa yakitekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) na kuratibiwa na Kurugenzi ya Miundombinu chini ya Wizara OR- TAMISEMI. 

Alisema kuwa Kuanzishwa kwa TARURA kunatenganisha majukumu ya kiutekelezaji na yale ya usimamizi na TARURA inategemewa kutekeleza majukumu yake kwa kuzingatia misingi ya ki-biashara, ufanisi wa gharama (Cost Effectiveness), masuala mtambuka (mazingira, usalama, na masuala ya kijamii) kwa ajili ya maendeleo endelevu ya kijamii na ki-uchumi. 

Alisema kuwa TARURA Mkoa wa Iringa inahudumia mtandao wa barabara wenye jumla ya Kilomita 4601.25 inayojumuisha Halmashuri tano ambazo ni Iringa Manispaa, Halmashauri za wilaya za Iringa, Kilolo, Mufindi na Mji wa Mafinga. 

“TARURA Mkoa wa Iringa ilitangaza miradi ya barabara ya halmashauri zote za Mkoa, jumla ya Zabuni 26 yenye thamani ya Tsh 6.5 bilioni ambayo leo utaishuhudia Mikataba 18 ikisainiwa na Wazabuni walioshinda baada ya mchakato mzima wa manunuzi kukamilika yenye thamani ya Tsh 3.56 bilioni,” alisema Eng. Wambaura. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...