Skip to main content

WAETHIOPIA 83 WAPANDISHA KIZIMBANI




MAHAKAMA ya hakimu mkazi mkoa wa Iringa imewapandisha kizimbani watuhumiwa 83 raia wa nchini Ethiopia kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Wakisomewa mashataka yao mbele ya hakimu mkazi mfawidhi mkoa wa Iringa David Ngunyale wakili wa serikali Godfrey Ngwijo alisema kuwa Februari 23 katika tarafa ya Mazombe wilaya ya Kilolo mkoani hapa watuhumiwa hao walikamatwa na maofisa uhamiaji kwa kosa la kuingia nchini bila kibali.

Ngwijo alisema kuwa kosa la pili linamkabidhi utingo wa gari hilo Hassan Ferooz (18) mkazi wa Tukuyu mkoani mbeya kwa kosa la kusafirisha watuhumiwa hao kuwapeleka nchini Afrika kusini lakini mtuhumiwa huyo alikana shitaka hilo.

Kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza ambapo mara baada ya kusomewa mashtaka hayo hakimu Ngunyale alisema kwa kosa la kuingia nchini bila kibali ni kwamba kesi hiyo itatajwa tena Machi mbili mwaka huu hadi watakapopata mtafsiri ambaye atatafsiri raia hao huku kosa la pili likiwa ni kwamba mtuhumiwa kosa lake linadhaminika.

Awali kabla ya kuanza kwa kesi hiyo raia hao walionekana wakiangua vilio mahakamani hapo hali ambayo ilimlazimu hakimu kumtaka mwanasheria wa serikali kumtafuta kiongozi wao kwa lengo la kuwatuliza jambo ambalo lilifanikiwa.

Ngwijo alisema Februari 23 mwaka huu raia hao wasio na vibali walikamatwa wakiwa na gari aina ya lori lenye namba za usajili T.903 AKH ,Mali ya Gabriel G.Mwakyambiki wa tukuyu mkoani Mbeya.

Hata hivyo Februari 21 mwaka huu raia wengine wanne wa nchini Ethiopia walikamatwa na idara ya uhamiaji wakiingia nchini bila kibali ambapo ofisa uhamiaji wa Iringa Hope Kawawa alisema kuwa Iringa sio uchochoro wa kupitisha raia wasio na kibali.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...