Skip to main content

WILAYA YA KILOLO YATENGA HEKTA 72.3 KWA AJILI YA UWEKEZAJI


Image may contain: 4 people, people sitting, table and indoor

Image may contain: 1 person, indoor

Kampeni ya uanzishaji wa viwanda kote wilayani Kilolo Mkoani Iringa imezinduliwa jana huku mwito zaidi ukielekezwa kwa umma kutoa ushirikiano kwa timu ya wataalamu katika kutekeleza mradi wa viwanda. 

Mkuu wa wilaya ya Kilolo Asia Abdalla alisema eneo lenye ukibwa wa hekta 72.3 limetengwa kwa ajili ya viwanda huku akiwataka wananchi kuchangamkia fursa hiyo. 

Kampeni ya uanzishaji wa viwanda kote wilayani Kilolo Mkoani Iringa imezinduliwa huku mwito zaidi ukitolewa kwa wananchi kujiunga kwenye vikundi kujisajili na kutoa ushirikiano kwa timu ya wataalamu itakayochunga mwenendo wa viwanda vidogo. 

Abdalla alisema eneo lenye ukibwa wa hekta 72.3 limetengwa kwa ajili ya viwanda huku akiwataka wananchi kuchangamkia fursa zikiwamo za uchakataji wa mazao ya misitu na mashambani. 

Hadi sasa wilaya ya Kilolo inakadiliwa kuwa na viwanda 22 , Hatua hii ya uzinduzi inajiri baada ya 

Mkoa wa Iringa kuzindua mwishoni mwa mwaka uliopita kwa minajili ya utekelezaji wa agizo la 

Waziri wa Tamisemi seleman Jaffo la kutaka ifikapo baadae mwezi Disemba kila mkoa kuwa na viwanda 100. 

Asiah Abdalla anahimiza umoja kuelekea utelezaji wa azma ya serikali kuufikia uchumi wa kati kwa kupitia sekta ya viwanda. 

Mkuu wa wilaya anasema kulingana fursa zilizopo wilayani humo ikiwa mazao ya mashambani na misitu, shughuli za ujenzi kunauwezekano mkubwa wa kuanzisha viwanda. 

Baadhi ya wadau wakiwamo sekta ya fedha wanawaambia wajumbe wa kikao hiki muhimu kwa utekelezaji wa azma ya serikali ya kila mkoa lazima kuwe na viwanda mia moja kwamba mitaji si tatizo maadam wajisajiri tu. 

Mkutano wa wadauwa dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi wilayani kilolo waliandaa kikao hicho kichoambatana na uzinduzi wa kampani ya ‘Wilaya yetu, Viwanda vyetu’ yakuchochea wananchi kushiriki kikamilifu kwa ujenzi wa uchumi wa viwanda. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...