Skip to main content

PAROKIA YA MTANDIKA KUSHEREHEKEA PASAKA KWA MWANGA




Meneja Selebu Rocks Spring Water Ltd Edgar Lamba (kulia) akikabidhi msaada wa vifaa vya umeme jua (solar panel kits) kwa Paroko Fr. Silvanus Ndazi wa Parokia ya Mtandika, Jimbo Katoliki Iringa jana.  



KILOLO: Parokia ya Mtandika katika Jimbo Katoliki Iringa wilayani Kilolo mkoani Iringa itasherehekea Siku Kuu ya Pasaka kwa mwanga baada ya kupata msaada wa umeme wa nishati ya jua (solar panel kits) kutoka Selebu Rocks Spring Water Ltd Wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa.

Msaada huo wenye thamani shilingi milioni 6.9 ni mchango kutoka kwa mkurugenzi na mfanyabiashara mkongwe Mzee John Lamba wa Kiwanda cha maji wilayani kilolo, mkoani Iringa.

Akizungumza jana wakati wa kukabidhi vifaa hivyo vya umeme wa jua, Meneja Selebu Rocks Spring Water Ltd Edgar Lamba kwa niaba ya mkurugenzi na mfanyabiashara mkongwe Mzee John Lamba alisema kuwa wamesukumwa kutoa vifaa hivyo ili kuwezesha upatikanaji wa huduma za kiroho nyakati zote na kuzingatia kuwa Parokia ya Mtandika haijafikiwa na umeme wa Gridi ya Taifa.

“Parokia ya Mtandika inakabiliwa na changamoto ya umeme kwa muda mrefu sasa…,” alisema meneja huyo.

Alisema kuwa kampuni hiyo imetoa msaada wa nishati ya umeme wa jua ili waumini wa parokia hiyo pamoja na mapadre washerehekee Siku Kuu ya Pasaka kwa mwanga.

Lamba aliongeza kuwa Parokia ya Mtandika ipo mbali na gridi ya umeme wa Taifa hivyo kukosa huduma hiyo muhimu ya umeme na kuongeza kuwa umeme huo utawekwa pia katika nyumba ya mapadri.

Akitoa salamu za shukrani kwa niaba ya Parokia ya Mtandika Paroko Fr. Silvanus Ndazi alishukuru kwa msaada huo wa nishati ya umeme ya jua na kuongeza kuwa waumini wa parokia hiyo watasherekea siku kuu ya Pasaka kwa mwanga wa uhakika.

Alisema kuwa parokia nyingi zilizopo maeneo ya vijijini ambazo hazijafikiwa na umeme wa gridi ya Taifa zimekuwa zinasherekea siku kuu wakati wa usiku kwa kutumia vibatari, taa na tochi jambo ambalo limekua linahatarisha usalama. 

“Lakini leo tumepata ufumbuzi wa mwanga kwa hiyo waumini watasherekea Siku Kuu ya Pasaka ambayo ni siku maalum ya kumbukumbu ya kufufuka kwa Yesu Kristo,” alisema Fr. Salvanus.


Jimbo la Katoliki Iringa lipo chini ya Askofu wa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa ambaye pia Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).Na Friday Simbaya, Kilolo

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...