Skip to main content

WAWILI WASHIKILIWA KIFO CHA MWANAFUNZI



IRINGA: JESHI la polisi mkoani Iringa linawashikilia watu wawili kuhusiana na tukio la kifo cha kiutatanishi cha mwanafunzi wa shule ya sekondari Mwembetogwa kilichotokea juzi maeneo ya mtaa Kisiwani kata ya Mwangata manispaa ya Iringa. 


Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa ACP, Juma Bwire akizungumzia tukio hilo juu ya tukio la kifo cha mashaka kilichotekea majira ya saa 12 asubuhi ambapo mwanafunzi wa kidato cha sita Sudi George (22) mkazi wa Kisiwani alikutwa amefariki dunia kwenye miti ya kugema pombe ya ulanzi huku mwili wake ukiwa na kamba maeneo ya shingoni. 


Kamanda Bwire alisema majina ya watu hao hawezi kuwataja lakini inaonyesha kuwa taarifa za awali zinaonyesha kuwa Machi 12 marehemu akiwa na sare za shule alitoka kwao kuelekea shuleni lakini hakurudi hadi mwili wake ulipopatikana katikamaeneo hayo. 


Alisema kuwa baada ya taarifa za tukio hilo kufika jeshi la polisi walifanya msako mkali kuhusiana na tukio hilo na kufanikiwa kuwakamata watu wawili ambao wako nje ya familia kutokana na mazingira ambayo yalijitokeza na taarifa walizopata. 


Alisema kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi mkali kubaini chanzo cha tukio kilichopelekea mwanafunzi huyo kukutwa katika hali hiyo pamoja na kupata taarifa za kitibabu hivyo taarifa kamili itafuata baada ya kukamilisha upelelezi. 


Kamanda Bwire alitoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuweza kubaini nani anahusika zaidi na tukio hilo na kuwataka wananchi kuachana na matendo ambayo yanahusiana na imani za kishirikina. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...