Skip to main content

WORLDSHARE KUJENGA HOSTELI YA WASICHANA KUPUNGUZA MIMBA SHULENI








Shirila lisilo la kiserekali la WorldShare toka Korea Kusini limeanza ujenzi wa hosteli ya wasichana katika Shule ya sekondari Kidamali iliyopo katika kata ya Nzhi wilayani Iringa, mkoani Iringa ilikupunguza tatizo la mimba kwa wanafunzi wa kike. 

Hayo yalifahamika jana wakati Mkuu wa Shule ya Sekondari Kidamali Sixtus Kanyama alipokuwa anatoa taarifa ya shule hiyo kwa maafisa toka ubalozi wa Korea Kusini na maafisa wa shirila la worldshare na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

Alisema kuwa shule hiyo inakabiliwa na tatizo la mimba kwa watoto wa kike kutokana na kutokuwepo hosteli ya wasichana ambapo wanafunzi wanalazimika kupanga vyumba mitaa na kukumabana na vishawishi mbalimbali. 

Kanyama alisema kuwa Shule ya Sekondari Kidamali inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo mimba kwa watoto wa kike kwa kuwa wingi wao wamepanga vyumba na kuishi pekee yao bila ulinzi. 

Alisema kuwa wanafunzi wengi wanatembea umbali mkubwa kwenda shule na kuridi takriban kilometa 40 kila siku na kupelekea kuongezeka kwa utoro mkubwa na kutojihusisha na masomo. 

Alisema kuwa kutokuwepo na hosteli kwa wanafunzi kumepelekea mdondoko kuwa mkubwa hasa kwa wanafunzi wa kike ambao husababishwa na vishawishi vya wanaume na kufanya mazingira ya shule kutovutia kuendelea na shule. 

Aidha, Mwalimu Mkuu huyo alisema kuwa wanafunzi wengi wakiwemo wa kike wanajihusisha na makundi rika yenye tabia hatarishi na kuongeza kuwa wastani wa mimba 16 zinaripotiwa kila mwaka katika shule hiyo. 

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt Augustine Mahiga ambaye aliambana na maafisa wa Ubalozi ya Korea Kusini na maafisa wa WorldShare, alilishukuru Shirika la Worldshare kwa kukubali kujenga bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Kidamali. 

Alisema kuwa hosteli ni jibu kwa matatizo hayo, kwa kuwa zipo faida nyingi za wanafunzi kukuishi bwenini na kuzitaja faida hizo kuwa ni pamoja na wanafunzi wa kike watakuwa alama kwa kuwa watakuwa chini ya matroni na walimu. 

Dkt Mahiga alisema kuwa faida zingine kwamba wanafunzi watapata muda mwingi wa kujisomea, watapata malezi yanayofanana na kulindwa, wanafunzi wa kike wengi watafaulu na kujiunga na elimu ya juu. 

Alisema kuwa hosteli inayotarajia kujengwa hapo shuleni itapewa jina la ‘Nara Memorial Dormitory’ ambapo ‘Nara’ kwa luhga ya kikorea ina maana ya nchi, Nara ni mwanzishi wa wazo la kujenga hosteli ya wasichana katika shule ya kidamali, lakini amekufa kabla wazo lake halijatimia. 


Naye, Dada Mkuu wa Shule ya Sekondari Kidamali Emmi Mkupasi alilishukuru Shirika la Worldshare toka Korea Kusini pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje Dkt Mahiga kwa kuwatafuta wadau hao kuja kuwajengea hosteli ya wasichana. 

Alisema kuwa uwepo wa hosteli ya wasichana kutasaidia kupunguza tatizo la mimba kwa wanafunzi wa kike kwa vile watoto wa kike wengi wanashinda kumaliza shule kutokana na changamoto nyingi ikiwemo tatizo la mimba. 

Dada mkuu Mkupasi kutoka kidato cha cha tatu aliongeza kuwa wapo wanafunzi walioanza nao kidato cha kwanza lakini waliaacha shule kwa sababu ya mimba kwa vile wanafunzi wengi wamepanga vyumba mitaani. 

Naye mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Robert Masunya ambaye aliongozana na wataalamu mbalimbali wa halmashauri hiyo akiwemo Diwani wa Kata ya Nzihi, Stephan Mhapa, alishukuru shirika hilola worldshare kutoka korea kusini. 

Alisema kuwa shule ya kidamali ya sekondari inakabiliwa na changamoto ua ukosefu wa makataba, ukosefu wa ukumbi wa mikutano, maabara ya za masomo ya sayansi ambazo zipo lakini hazijamalika kujengwa na vyoo vilivyopo vyote matundu 16 ni chakavu. 

Masunya alisema kuwa changamoto zingine ni nyumba za walimu, maabara ya TEHEMA, na kisima cha maji. 

Hata hivyo, Shirika la WorldShare toka Korea kusini limekubali kujenga hosteli ya wasichana pamoja na kujenga fensi ya kuzunguka bweni hilo, kujenga vyoo na kuchimba visima vya maji ilikutatuwa tatizo la maji shuleni hapo. 

Shule ya sekondari kidamali ni shule ya kata ambayo kwa kiasi kikubwa imejengwa kwa nguvu za wananchi. Shule iko taarifa ya kalenga, kata ya nzihi na kidamali. 

Shule hii ilifunguliwa tarehe 30.05.2005 ikiwa na wanafunzi 76; wavulana 40 na wasichana 36, kwa sasa shule ina wanafunzi 600 kati yao wasichana 368 sawa na asilimia 61 na wavulana 232 sawa n asilimia 39 ya wanafunzi woyte. 

Shule hiyo ina walimu wako 35, wakikie 15 na wakiume 20 na ina wa ekari 15.84. Shule ya sekondari kidamali inahudumia jumla ya vijiji vine ambavyo ni Kipera, Nyamihuu, Nzihi na kidamali. Na Friday Simbaya, Iringa 





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...