Skip to main content

MAGUFULI MGENI RASMI MEI MOSI MKOANI IRINGA



Mshambuliaji Ramadhani Madebe (23 jezi nyekundu) wa Uchukuzi akiwa katika msitu wa wachezaji wa timu ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Joseph Mlimi (2), Mohamed Koshuma (16) na Stephen Mgendi (12) katika mchezo wa michuano ya Mei Mosi uliofanyika kwenye uwanja wa Samora. Uchukuzi walishinda bao 1-0. (Picha na Bahati Mollel wa TAA). 



Winga Salum Idd wa Tumbaku ya Morogoro (11) akikokota mpira kuelekea langoni mwa Tanesco wakati wa mchezo wa michuano ya Kombe la Mei Mosi uliofanyika jana kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa. Tumbaku walishinda mabao 2-0. (Picha na Bahati Mollel wa TAA).








Kikosi cha timu ya soka ya Uchukuzi kikiwa pamoja na kocha wake Mkuu Zenno Mputa (kulia) na Mshauri wa timu Kennedy Mwaisabula (Mzazi), kinachoshiriki katika michuano ya Kombe la Mei Mosi inayofanyika katika viwanja mbalimbali mkoani Iringa. (Picha na Bahati Mollel wa TAA).




IRINGA: Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza ameomba wafanyakazi wote na wananchi kwa jumla kujitokeza kwa wingi kumlaki Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kupokea salamu zake za Mei Mosi katika Uwanja Samora. 

Alisema kuwa Mkoa wa Iringa umechaguliwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya kitaifa ya sherehe za siku ya wafanyakazi duniani yaani MEI MOSI mwaka 2018. 

Maadhimisho ya mwaka huu yanaogozwa na kauli mbiu isemayo kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii kulenge kuboresha mafao ya mfanyakazi. 

Masenza alisema kuwa kilele cha maadhimisho ya mei mosi mwaka 2018 kitakuwa katika uwanja wa michezo wa kumbukumbu ya Samora, mjini Iringa ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. 

Maadhimisho ya sherehe za mei mosi yatanguliwa na michezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mpira wa miguu, mpira wa pete, kamba, bonaza la michezo mbalimbali. 

Michezo hii ilianza tangu tarehe 17/04/2018, na itaitimishwa tarehe 30/04/2018. 

Aidha, mkuu wa mkoa huyo aliongeza kuwa sherehe za mei mosi zitahusisha maonesho ya shughuli, huduma na bidhaa mbalimbali za wafanyakazi, taasisi za umma na binafsi, wawekezaji za wajasiriamali katika Uwanja wa Kichangani uilopo eneo la Kihesa mjini Iringa. 

Maandalizi ya sherehe za mei mosi yanaendelea vizuri, kamati mbalimbali zimeundwa kwa maandalizi ya shughuli zote zitakafanyika kabla na wakati wa maadhimisho hayo. 

Kwa upande wake, Kaimu Mweneyekiti michezo ya Mei Mosi Kitaifa Joyce Benjamin ameupongeza Mkoa wa Iringa kwa maandalizi mazuri ya sherehe za wafanyakazi duniani. 

Alisema kuwa amefurahishwa na maandalizi yaliofanywa na Mkoa wa Iringa na kuongeza kuwa hajawahikuona maandalizi kama hayo tangu aanzekushiriki maadhimisho ya Mei Mosi 2009 kwa ushirikiano mzuri. 

Joyce alisema kuwa timu mbalimbali zimewasili kushiriki michezo mbalimbali hayo timu za micchezo zimefika hapa Iringa kushiriki michezo ikiwa ni pamoja na mpira wa miguu, mpira wa pete, kamba, bonaza la michezo mbalimbali. 

Alisema kuwa michezo ni furaha na muhimu kwa wafanyakazi kwa vile inaleta afya na kushirikiano baina ya wafanyakazi na hatimaye kuleta umoja ya kitaifa. Na Friday Simbaya, Iringa 




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...