Skip to main content

PANAMA QUEENS’ FC YA IRINGA YALIA NA UKATA



Kocha Mkuu wa timu ya Panama Queens FC, Miraji Fundi akizungumza na waandishi wa habari baada ya mechi yao dhidi ya Mlandizi Queens FC ya Pwani ambapo timu hiyo ilifungwa bao 5-2 katika Uwanja wa nyumbani wa Samora mjini Iringa Jumapili. (Picha na Friday Simbaya) 
Meneja wa timu ya Mlandizi Queens FC Yassin Ramadhani

Na Friday Simbaya, Iringa 

Timu ya mpira ya wanawake mkoani Iringa Panama FC inakabiliwa na changamoto lukuki ikiwemo la kukosa vifaa mbalimbali michezo kama vile mipra, imeelezwa. 

Akizungumza na Nipashe jana Kocha Mkuu wa timu ya Panama Queens FC, Miraji Fundi baada ya mechi yao dhidi ya Mlandizi Queens FC ya Pwani alisema kuwa timu yake inakabiliwa changamoto mbalmabli ilikiwemo la kukosekana kwa vifaa mbalimabi vya michezo pamoja na kutoungwa mkono na wadau mpira wa wanawake mkoani hapa. 

Alisema kuwa kufanya vibaya kwa timu hiyo ligi ya soka ya wanawake Tanzania bara kunatokana na kutoungwa mkono na wadau pamoja na mwitikio mdogo kutoka kwa wanairinga na kuongeza kuwa wasipokaa vizuri wanaweza kukosa timu ya wanawake. 

Jana Jumpili (22/04/2018)timu ya Panama Queens iliikaribisha timu ya Mlandizi Queens ya mkoani Pwani katika uwanja wa nyumbani ambao pia ni mabingwa watetezi katika uwanja kumbukumbu wa Samora mjini Iringa na kuambulia kichapo cha magoli 5-2. 

Katika timu ya mabingwa watetezi ya Mlandizi magoli yalifungwa na Lucy Mrema aliyefunga magoli matatu, Annatazia Nyandago na Sabina Mbuga waliyefunga goli moja moja na kwa upande wa Panama FC magoli yote yalipachikwa kupitia kwa mshambuliaji Mgeni Kisoda. 

Fundi alisema kuwa timu yake inakabiliwa na ukata wa vifaa mbalimbali vya michezo ikiwemo mipra na fedha za kuweza kuiandaa timu hiyo inayoshirika ligi ya soka ya wanawake Tanzania (TWFA) hatua ya nane bora inayoendelea nchini. 

Kocha mkuu huyo aliongeza kuwa Timu ya Panama FC katika mechi yao ijao itamenyena na Simba Queens ya jijini Dar es Salaam ambayoitachezwa ugenini. 

Naye Meneja wa timu ya Mlandizi Queens FC Yassin Ramadhani alisema kuwa amefurahishwa na matokeo ya timu dhidhi ya Panama Queens FC kwa kuzoa alama tatu na kufanya timu kufikisha pointi tisa. 

Alisema kuwa timu ya Mlandizi Queens imekuwa ya kwanza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara baada ya kuifunga Panama FC ya Iringa kwa mabao 5-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam mwaka jana. 

Ligi ya soka ya wanawake hatua ya nane bora inaendelea nchini katika mtindo wa nyumbani na ugenini. 

Mwenyekiti wa chama cha soka cha wanawake Tanzania (TWFA) Amina Karuma, alisema ligi hiyoilisimama kupisha timu ya taifa ya wanawake (Twiga Stars) iliyokuwa ikiandaa na mechi zake mbili za kuwania tiketi ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya afrika dhidi ya Zambia lakini ilitolewa. 

Ligi hiyo inayochezwa kwa mtindo wa nyumbani na ugenini na kudhaminiwa na kampuni ya bia ya Serengeti. 

Karuma alisema kuwa ligi hiyo itasimama tena Mei 3 mwaka huu ili kupisha maadalizi ya Twiga Stars inayotarajia kushiriki mashindano ya kombe ya chalenji nchini Rwanda tarehe 11/05/2018. 

Mwisho 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...