Skip to main content

Uchukuzi, Tanesco soka zakaribia nusu fainali


Mchezaji Erick Mpunga wa Uchukuzi (kulia) akijaribu kuzuia mpira unaotaka kupigwa na Kassim Mdee wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu (NAO) katika mchezo wa mpira wa miguu wa michuano ya Kombe la Mei Mosi uliofanyika jana kwenye uwanja wa Samora mkoani Iringa. (Picha na Bahati Mollel wa TAA).



IRINGA: TIMU za soka za Uchukuzi na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) zilizopo kundi ‘A’ na ‘B’ zinakaribia kutinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mei Mosi baada ya jana kushinda michezo ya iliyofanyika kwenye uwanja wa Samora, ambapo kila mmoja zinaongoza kundi lake kwa kujikusanyia pointi sita. 

Uchukuzi inafuatiwa na mabingwa watetezi Geita Gold Mine (GGM) wenye pointi mbili, NAO na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro yenye pointi moja kila mmoja; wakati Tanesco inafuatiwa na Tumbaku nayo inapointi sita lakini imezidiwa magoli ya kufunga, huku RAS Iringa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro wakiwa hawana pointi. 

Katika mechi hizo za jana Uchukuzi waliwafunga Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu (NAO) kwa magoli 3-1. Nao ndio walikuwa wa kwanza kupachika bao katika dakika ya 45 kupitia kwa Peter Dihoko aliyeunganisha kona ya George Mlelwa. 

Uchukuzi walisawazisha katika dakika ya 60 kupitia wa Kado Nyoni, huku bao la pili lilifungwa na Omary Kitambo dakika ya 63 na bao la tatu dakika ya 68 lililofungwa na Issack Ibrahim. 

Nao Tanesco waliwachapa RAS Iringa kwa magoli 4-0, ambapo matatu yaliyofungwa na Kurwa Mangara katika dakika ya 19, 34 na 59 huku Salehe Bakari alifunga bao la nne dakika ya 66. 

Katika mchezo wa netiboli timu ya RAS Iringa iliwafunga Tanesco kwa magoli 27-14. Washindi walikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa magoli 9-7. Nayo Ikulu walipewa ushindi wa mezani wa magoki 40 na pointi mbili baada ya Malaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kushindwa kufika uwanjani Chuo Kikuu cha Katoliki (RUCU) kwa kuwa na majeruhi wengi waliotokana na kuvuta kamba. 

Katika mchezo wa kuvuta kamba kwa wanawake timu ya Uchukuzi ilivutwa na RAS Iringa 1-0 baada ya mvuto wa awali kutoka sare; huku kwa upande wa wanaume wa Uchukuzi waliwavuta Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu (NAO) kwa mivuto 2-0. 


Wachezaji wa timu ya wanawake ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kulia wakiongozwa na Neema Mbuja wakiwavuta wenzao wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) jana kwenye michuano ya Kombe la Mei Mosi uliofanyika uwanja wa Samora. Tanesco walishinda kwa mivuto 2-0. (Picha na Bahati Mollel wa TAA).


Michezo mingine ya kamba wanawake walivutwa na MUHAS mivuto 2-0; nayo NAO waliwavuta Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mvuto 1-0 kwa upande wa wanaume. 

Michuano hiyo inaendelea leo kwa upande wa netiboli timu ya Uchukuzi itacheza na RAS Iringa uwanja wa RUCU; huku katika soka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro watgakuna na Tumbaku ya Morogoro, na GGM watacheza na Uchukuzi kwenye uwanja wa Samora; wakati katika kamba RAS Iringa kuumana na Tanesco kwa wanawake. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...