Skip to main content

DC MUFINDI: VIJANA WA JKT MSITUMIE MAFUNZO MLIOPATA VIBAYA



Kikundi cha Singe cha vijana wakijitolea kundi Mererani 2018 wakipita mbele ya mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri William wakati wa mahafali ya kumaliza mafunzo ya awali ya jeshi la kujenga taifa (JKT) kikosi cha Maginga JKT wilyani Mufindi, Mkoa wa Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)





MUFINDI: MKUU wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri William amsema vijana wanaohitimu mafunzo ya awaliya kijeshi la jeshi la kujenga taifa (JKT) kuyatumia mafunzo wanayoyapata katika kambi mbalimbali hapa nchini kwa faida ya Taifa. 

Hatua hii inaelezwa kuwa kama itazingatiwa na vijana wanaohitimu mafunzo ya muda mfupi ya JKT upo uwezekano mkubwa wa taifa kuwa na vijana ambao watakuwa waadilifu pindi watakapokuwa wakilitumikia taifa. 

Akizungumza na wahitimu hao jana Mkuu wa Wilaya ya Mufindi Jamhuri Wiliam aliwataka kuyatumia vizuri mafunzo na maarifa waliopata katika kuliletea taifa maendeleo. 

Awali, wakisoma risala yao mbele ya mgeni rasmi wahitimu hao waipongeza serikali kwa kuyarudisha mafunzo ya JKT na kusema kuwa yatasaidia katika kurudisha umoja wa kitaifa ambao kwa siku za karibuni umekuwa ukilegalega. 

Akisoma risala hiyo kwa niaba ya wahitimu, Ramadhan Mohammedi akisaidiwa na Magdalena Mniko alisema kuwa mafunzo hayo ya awali ya kijeshi ya kujitolea kundi- Mererani, yalifunguliwa rasmi tarehe 22 Januari, 2018 na kamanda kikosi 514 KJ makambako kanali J.L Kashinde, ikiwa na vijana 1,185 kati yao wavulana 815 na wasichana 370. 

Mohamedi alisema mpaka kufikia jana kosi imefikia wiki ya 24 ambayo ni wiki mwisho ya mafunzo hayo ya awali idadi ya kuruta 1,179 na wengine sita (6) hawakufanyiwa kuhitimu mafunzo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kushindwa uvumilivu, uvivu, kukosa ustahimilivuwa moyo na uzalendo kwa nchi yao. 

Alisema kuwa katika kipindi cha cha mafunzo walijifunza stadi za maisha kama vile shughuli za kilimo, ufugaji, ujenzi pamoja na shughuli zingine za uzalishaji mali na kazi mbalimbali za kijamii. 

Kwa upande wake, kaimu kamanda kikosi Kikosi cha Mafinga JKT Kapteni Victor Nkya alielezea kuwa mafunzo ya awali kwa vijana waliohitimu katika kambi hiyo kuwa yenye mafanikio makubwa kutokana na mbinu mpya zilizotumika katika kuhakikisha vijana wote waliojiunga na mafunzo hayo wanayamaliza salama. 

Nkya alisema kuwa mafunzo hayo yalilenga kuwajenga ama kuwafundisha mambo mbalimbali kama vile uzalendo kwa nchi yao, upendo, umoja, mshikamano na ushirikiano, uvumilivu na ushapavu, nidhamu na ujasiriamali. 

Alisema kuwa kwa ujumla wao vijana wamepikwa na wameiva na wamepata mafunzo na malezi kwa mujibu wa muongozo wa mafunzo ya kujitolea. 

Jeshi la Kujenga Taifa lilianzishwa Julai 10, 1963 na serikali kwa lengo la kuwaweka pamoja vijana wa nchi hii na kuwapa malezi kuhusu uzalendo na umoja ili kuondoa dalili za matabaka zilizoanza kujitokeza katika jamii baada ya uhuru. 

Baadhi ya sababu za kuanzishwa kwa JKT ni: Kubadili fikra za vijana wa nchi hii kutoka ile hali ya ukoloni kutegemea nchi nyingine kuleta maendeleo. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...