Skip to main content

IRINGA KUKABILIANANA CHANGAMOTO ZA MTOTO WA KIKE KATIKA HEDHI


Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza akizungumza na wanafunzi wa Shule mbalimbali katika Manispaa ya Iringa wakati wa maadhimisho ya siku ya hedhi duniani yaliyofanyika mkoani Iringa jana. Julia kwake ni mganga mkuu wa mkoa wa Iringa Dkt Robert Salim na kushoto kwake ni mkurugenzi wa shirika la Afya Plus Suzan Yumbe. (Picha na Friday Simbaya)

Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza (mwenye hijab ya jano na miwani) akicheza muziki na wanafunzi wakati wa maadhimisho ya siku ya hedhi duniani waliofanyika mkoani Iringa jana. (Picha Friday Simbaya)




SERIKALI mkoa wa Iringa umelenga kuwawezesha wasichana kutimiza ndoto za maisha yao kwa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowafanya wabaki nyuma katika kuhudhuria masomo kipindi wakiwa katika hedhi.


Hayo yamezungumzwa na mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza wakati wa kuelekea maadhimisho ya Siku ya Hedhi Duniani ambapo kimkoa yalifanyika kwa mara ya kwanza jana katika Bustani za Manispaa na kuhudhuriwa na wanafunzi wa kike kutoka shule mbalimbali za sekondari za mjini hapa ambapo kila mwaka yanaadhimishwa Mei 28.


Alisema kuwa changamoto kubwa ambayo wanakabiliana nayo watoto wa kike wengi walioko mashuleni ni kipindi cha hedhi ambapo baadhi yao wamekuwa hawana elimu, kutojiamini na utoro mashuleni wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi hali inayosababisha utoro.


Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano inayo dhamira ya dhati kuhakikisha elimu bure inapatikana kwa jinsia zote hivyo basi suala la hedhi salama kwa wa kike ni jambo la msingi katika ngazi ya familia, jamii, na hata mashuleni kuwapatia elimu itakayowezesha kuwa na ufahamu wa masuala ya hedhi.


Masenza alisema kuwa ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha kuwa mtoto wa kike anahudhuria masomo yake kwa mwaka mzima pasipo kuwa na vikwazo vinavyosababishwa ama na mazingira duni au ukosefu wa bajeti katika kupata taulo hizo maalum za hedhi.


Aliwataka wadau na wananchi kwa ujumla kuvunja ukimya juu ya suala la hedhi salama kwa mtoto wa kike na kuwezesha mtoto wa kike kupata taulo maalum kila mwezi na mkoa wa Iringa una mkakati maalum wa kumaliza changamoto hizo.


“Changamoto mbalimbali zinazowakabili wasichana wanapokuwa kwenye vipindi vya hedhi yanapaswa kujadiliwa na kutafutiwa ufumbuzi wa kudumu kwa kuwa yanachangia kurudisha nyuma jitihada za kuwainua watoto wa kike nchini na kuwataka mabinti kuondoka na aibu ya katika suala la hedhi hivyo mkakati upo kumaliza kwa kuwapatia bure mataulo maalum watoto wa kike” alisema


Awali Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Afya Plus, Suzan Yumbe ambao ndio waratibu wa maadhimisho hayo mkoa, alisema kuwa lengo la maadhimisho hayo ni kuvunja ukimya juu ya masuala ya hedhi ikiwemo kuondokana na dhana potofu kwamba hedhi ni ugonjwa pamoja na namna bora ya kuhakikisha mtoto wa kike anajiweka katika hali ya usafi ili abaki shuleni badala ya kukosa masoko kila apatapo hedhi.


Alisema ukosefu wa mazingira bora kama vyoo, maji safi na salama pamoja na vyumba mahsusi vya kubadilishia nguo , hasa kwa watoto wa kike wanapokua katika hedhi mashuleni kuna changia utoro.


Alisema kuwa shirika hilo tangu limeanza kutoa elimu ya hedhi wamekwisha gawa zaidi pedi 600 kwa wanafunzi wa kike mbalimbali katika shule mbalimbali mjini hapa na kuwezesha kupunguza kwa kiasi kikubwa utoro mashuleni.


Yumbe alisema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yanaambatana na kauli mbiu ya ‘Hakuna vikwazo zaidi wezesha wanawake na wasichana kupata hedhi salama’ hivyo shirika hilo lina mikakati ya kuwezesha watoto wa kike kupata taulo maalum za kufua na kuzitumia tena ambazo ni salama na zitamwezesha mtoto kike kuhudhuria masomo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...