Skip to main content

ZIMAMOTO YAWATAKA MAKAMPUNI KUWA NA FIRE PROTECTION MANAGERS WA MOTO



Kamishna Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye (mwenye kaunda suti) akizungumza na viongozi mbalimbali wa jeshi hilo wakati wa maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pakazi nchini ambayo huadhimishwa duniani kote tarehe 28 Aprili kila mwaka, yaliofanyika mkoani Iringa. (Picha na Friday Simbaya)



IRINGA: Kamishna Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, Thobias Andengenye ametoa wito kwa makampuni na wenye viwanda nchini kuwaajiri wataalamu wa moto (fire protection managers) watakaobaini na kung’amua na kukinga moto katika maeneo yao. 

Alisema kuwa makampuni na viwanda kwa kushirikiana jeshi hilo wanatakiwa kuwaajiri wataalamu wa mambo ya moto kwa lengo la kubaini endapo moto utatokea katika maeneo ya kazi. 

Alisema kuwa wataalamu hao wa mambo ya moto wanatakiwa kupata mafunzo kutoka jeshi hilo ama mahali pengine kwa ajili ya kung’amua na kuzuia moto katika viwanda vyao na makampuni. 

Andenenye alisema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pakazi nchini ambayo huadhimishwa duniani kote tarehe 28 Aprili kila mwaka, yaliofanyika mkoani Iringa. 

Kamishna huyo hivi karibuni alitembelea banda la zimamoto na kukagua vifaa mbalimbali vya kuzimia moto wakati wa maadhimisho hayo yaliofanyika mkoani hapa. 

Maadhimisho haya huratibiwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) nchini na kwa mwaka huu yamefanyika Mkoani Iringa yakitanguliwa na maonyesho kutoka kwa wadau kuanzia tarehe 26 Aprili na kufikia kileleni leo tarehe 29. 

Mgeni Rasmi katika kilele cha Siku ya Usalama na Afya Mahala pa Kazi Duniani Mhe. Jenista Mhagama (MB) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu. 

Andengenye alisema kuwa jeshi hilo lilishiriki maonesho hayo ilikuwapa wananchi fursa ya kulijua jeshi lao la zimamoto na uokoaji ambalo lipo chini ya wizara ya mambo ya ndani nchini. 

Aidha, kamishna huyo alitoa kwa wananchi kuhakikisha wanapotaka kujenga nyumba zao za biashara au viwanda kuhakikisha wanapoleka ramani zao ili jeshi la zimamoto na uokaoji ilikague kama ramani hizo zina mifumo ya maji kuzimia moto. 

Hata hivyo, Adengenye alitoa wito kwa mamlaka mbalimbali kwa kushirikiana jeshi hilo kujenga visima vya maji katika maeneo mengi zaidi ili kusaidia jeshi hilo kuzima moto kwa haraka. 

Pia alisema kuwa wenye viwanda na kwenye maghorofa wanatakiwa kupeleka ramani zao kabla hawajaanza ujenzi ili kuaangalia kama rani hizo zina mifumo ya maji kwa ajiri yakuzimia moto. 

Mwisho 



Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...