Skip to main content

MEYA AWAPONGEZA WADAU WA MAENDELEO




Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Alex Kimbe amewaomba wadau mbalimbali kuchangia sekta za elimu, afya na maji pamoja sekta zingine katika manispaa hiyo. 

Meya huyo alitoa kauli hiyo jana wakati akifunga mkutano wa kawaida wa baraza la madiwani la manispaa ya iringa kwa kipindi cha robo ya tatu kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Kimbe alisema kuwa wadau wa maendeleo wanaweza kupunguza changamoto mbalimbali zinazoikabilia manispaa hiyo ikiwemo changomto yakutekamilika kwa badhi ya miradi ya maendelea kutokana na uhaba wa fedha. 

Alisema kuwa halmashauri ya manispaa ya iringa imewapongeza wadau mbalimbali wa maendeleo ikiwemo kampuni ya ASAS Group kwa kuchangia fedha katika sekta ya afya, maji na elimu. 

“Wakati tunalekea katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka 2017/18 kuna miradi mingi haijakamilika kutokana na uhaba wa fedha na sisi kama halmashauri tunatakiwa kujipanga kuweza kumalizia miradi ambayo haijakamilika,” alisema Kimbe. 

Katika hatua nyingine, kaimu mwenyekiti wa kamati ya kudhibiti ukimwi Halmashauri ya Manispaa Iringa Ibrahimu Ngwada alisema katika kipindi cha robo ya tatu, januari hadi machi 2017/2018 kamati hiyo ilieendelea kutekeleza mikakati ya kupambana na janga la ukimwi kwa kushirikiana na wadau wa mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI. 

Alisema kuwa huduma za ushauri na upimaji wa hiari zilitolewa, jumla ya watu 4269 wakiwemo wanaume 2145 na wanawake 2124 walipimwa afya zao kwa hiari. 

Ngwada aliongeza kuwa waliokutwa na maambukizi ya VVU/UKIMWI ni watu 383 kati yao wanaume 146 na wanawake 237. 

Aidha, kaimu mweneyekiti huyo alisema kuwa huduma za tiba sahihi ya magonjwa ya ngono ilitolewa katika vituo vyote vya afya na zahanati, ambapo jumla ya watu 325 wakiwemo wanaume 63 na wanawake 262 walipata tiba sahihiya magonjwa ya ngono. 

Wakati huohuo, Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela ambaye pia ni mshauri katika baraza la madiwani alitoa ushauri kwa baraza hilo kutatua migororo ya viwanja. 

Alisema tatizo la viwanja la double allocation ni kubwa kwa kuwa viwanja hivyo vinadaiwa kuwa mkoa unatoa viwanja na manispaa nayo intoa viwanja, yaani kiwanja kimoja kugaiwa mara mbili. 

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Wilaya huyo alisema kuwa rais Dkt John Pombe Magufuli anatarajia kuwa mgeni rasmi katika siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani yatakayofanyika kitaifa mkoani Iringa hapo tarehe 26.06.2018. 

Alisema kuwa rais Magufuli alivutiwa na mapokezi makubwa siku ya wafanyakazi duniani yaliyofanyika kitaifa mkoani Iringa. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...