Skip to main content

TANZANIA BADO INAKABILIWA NA CHANGAMOTO ZA MAZINGIRA



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam, juu ya maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani ambayo hufanyika Juni 5 kila mwaka.

WAKATI tukielekea katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani, Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa katika uhifadhi wa mazingira ambapo asilimia 61 ya nchi inakabiliwa na jangwa.


Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa Juni 5 kila mwaka.


“Tukielekea kwenye maadhimisho ya siku ya Manzingira Duniani, hali ya uhifadhi wa mazingira nchini inachangamato kubwa, asilimia 61 ya nchi yetu inakabiliwa na jangwa,” amesema Makmaba.


Amesema sababu ya hali hiyo nikutokana na kilimo, ufugaji na uvuvu usioendelevu ambao umepelekea upotevu wa viumbe hai, kuaharibiwa kwa vyanzo vya maji, kupunguwa kwa tija za shughuli za uzalishaji mali na uharibifu wa mazingira.


Ameeleza kuwa hali hiyo imepelekea hata kutokea kwa magonjwa amabyo ahayakuwepo ambapo alitoa mfano ni kuwepo kwa ugonjwa wa malaria katika maeneo ya milimani tofauti na awali.


Akizungumzia maadhimisho hayo, waziri Makamba amesema lengo ni kuelimisha jamii, masuala mbalimbali yahusuyo mazingira, kuhamasisha jamii kushiriki kikamilifu kwenye shughuli za maadhimisho hayo, kuhamasisha jamii kuwa mstari wa mbele kuchukua hatua za kuhifadhi na kulinda mazingira ya maeneo yao.


Pia amesema ni kutoa fursa kwa jamii mbalimbali kufahamu wajibu wao wa kuzuia madhara kwenye mazingira yanayotokana na shughuli za kijamii wanazofanya na kuhamasisha jamii kuyafanya mazingira yao kuwa salama na masafi ili kila mtu afurahie hali hiyo katika maisha ya sasa na ya vizazi vijavyo ambapo kimataifa yanafanyika ichini India katika mji wa New Delhi huku kitaifa yakifanyika jijini Dar es Salaam.


Makamba amesema lengo la maadhimisho haya kitaifa kufanyika jijini Dar es Salaam ni kuwapa fursa wananchi wa jiji hilo ya kuelemishwa na kuhamasishwa kupambana na changamoto za uharibifu wa mazingira unaolikumba jiji hilo kama vile, mafuriko, uchafuzi wa mazingira utokanao na plastiki, kubomoka kwa kuta za fukwe za bahari ya hindi pamoja na utumiaji wa kiasi kikubwa cha nishati ya mkaa.


Amesema kutokana na changamoto mbalimbali zinazokabili uhifadhi wa mazingira nchini, kuelekea siku ya maadhimisho hayo kutatanguliwa na wiki ya mazingira itakayo zinduliwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Mei 31 hadi Juni 5, 2018 katika viwanja vya Mnazi Mmoja na kutakuwepo na maonesho ya nishati mbadala ya mkaa na Teknolojia.


Ameongeza kuwa wajasiriamali na wataalamu wa teknolojia ya nishati mbadala wa mkaa watatoa mafunzo kwa jamii na kuwahamasisha kutumia nishati mbadala ya mkaa na maadhimisho hayo yatafungwa na Rais John Magufuli siku ya kilele Juni 5, 2018.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...