Skip to main content

ASILIMIA 80 YA AJILI ZINAZOTOKEA NCHINI USABABISHA NA MAKOSA YA KIBINADAMU


Na Friday Simbaya, Iringa 

Hali ya usalama barabarani nchini imekuwa siyo nzuri na hivyo kugharimu maisha ya wananchi kwa kusababisha ajili ambazo zimekuwa na athari ya kusababisha ulemavu na vifo, imefahamika. 

Hayo yalisemwa jana na mkuu wa wilaya ya iringa Richard Kasesela wakati mafunzo ya usalama barabarani, usimamizi wa mazingira na masuala ya kijamii kwa wataalamu wa Tanroads yanayendelea kufanyika mkoani Iringa. 

Mafunzo hayo siku nne ni kwa ajili ya kukuza weledi wa wafanyakazi wa TANROADS katika kutatua changamoto wakati kutekeleza miradi ya barabara. 

Mkuu wa wilaya huyo kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa iringa Amina Masenza, alisema kuwa ilikupunguza matatizo hayo wakala wa barabara nchini (TANROADS) wanatakiwa kutoa elimu ya usalama barabarani kwa wananchi na hata kwa wafanyakazi wake katika kutambua maeneo hatarishi. 

Alisema kuwa baadhi ya sababu zinazosababisha ajali ni pamoja na makosa ya kibinadamu ambayo huchangia asilimia 80, ubovu wa barabara unachangia asilimia nane (8%) na ubovu wa magari ambao unachangia asilimia 12. 

Kasesela alivitaja vyanzo vikuu vya ajili kuwa ni pamoja na mwendokasi wa madereva, kulipita gari linguine kwenye mlima au kona kali, kutoheshimu alama za barabarani, utumiaji wa barabara sio zingatia sheria, kukosekana kwa alama za barabara ambazo huibwa au kugongwa na magari na kukusekana kwa michoro ya barabarani. 

Kwa upande wa usimamizi wa mazingira, alisema pia hali siyo nzuri sana kwa vile wadau wengi wamekuwa hawaoni umuhimu uliopo katika usimamizi wa mazingira kwa utekelezaji wa miradi ya barabara. 

“Ni mara nyingi sana kukuta mkandarasi anachimba kifusi au kokoto kwa ajili ya ujenzi wa barabara na kuaacha mashimo bila kuyarekebisha ili kupunguza athari zinazo weza kutokea kwa kuwepo mashimo hayo,” alisema Kasesela. 

Aidha unapotembelea barabara zetu utakuta takataka mbalimbali ambazo zimetupwa na wasafiri barabarani na wakati mwingine wasfiri kujisaidia ovyo pembezoni mwa barabara maarufu kama ‘kuchimba dawa,’ alisema. 

Pamoja na kuwepo matatizo mengi ya usimamizi wa mazingira katika utekelezaji wa miradi ya barabara, wataalumu wa TANROADS wanatakiwa kujengewa mikakati ya kuyapunguza. 

Katika masuala ya kijamii kumekuwa na changamoto za ukimwi, usalama na afya mahali pakazi na kuhamisha watu katika hifadhi ya barabara. 

Kasesela alisema kuwa changamoto hizo bila kuziwekea mikakati madhubuti zitaleta athari kubwa kwa jamii katika utekelezaji wa miradi ya barabara. 

Kwa upande wake, mkuu wa idara ya mazingiara na usalama TANROADS makao makuu Zafarani Madayi alisema kuwa mafunzo hayo ni utaratibu wa kawaida ambao tanroads imejiwekea kila mwaka. 

Alisema lengo kubwa la warsha hizo za kila mwaka ni kujenga weledi kwa watumishi wake katika kusimamia na kutekeleza masuala ya mazingira, kijamii na usalama barabarani. 

Madayi alisema hayo ni masuala mtambuka yanayokwnda sambamaba na utekelezaji wa miradi ya barabara kuu na za mikoa nchini. 

Alisema kuwa kwa kawaida mafunzo hayo hutolewa kikanda na sasa ni zamu ya kanda ya nyanda za juu kasini ambapo mkoa wairinga ndio mwenyeji. 

Madayi aliongeza kuwa warsha hiyo imejumisha washiriki kutoka TANROADS makao makuu na ofisi za TANROADS mikoa yote 26 nchini. 

Washiriki hao ni wataalumu w tanroads wanaohusika na masuala ya mazingira, usalama barabarani, kijamii/UKIMWI, utunzaji wa hifadhi ya barabara, usanifu, ujenzi na matengezo ya barabara, ukaguzi wa mahesabu, rasilimali watu, madereva, na wataalumu wengine. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...