Skip to main content

RITA WAANZA MAJARIBIO YA MPANGO WA VIFO MKOANI IRINGA



Na Friday Simbaya, Iringa 

Serikali kupitia wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kushirikiana na Shirika la Umoja la Mafaita la kuhudumia watoto (UNICEF) na taasisi ya Bloomberg Data for Health pamoja na wadau maendeleo wengine imeanza kutekeleza mpango wa majaribio wa kusajili vifo mkoani Iringa. 

Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Emmy Hudson alisema hayo jana wakati wa kikao cha hamasa kwa viongozi wa mkoa na wilaya kuhusu majaribio ya mpango wa usajili wa vifo. 

Alisema kuwa kwa mara pili, Mkoa wa Iringa umepewa nafasi yakutekeleza mpango wa majaribio ya usajili wa vifo baada ya kufanya vizuri katika mpango wa maboresho ya mfumo wa usajili wa vizazi kwa watoto walio umri chini ya miaka mitano. 

Hudson alisema kuwa mkoa wa Iringa baada ya kufanya vizuri katika mpango wa maboresho ya mfumo wa usajili wa vizazi kwa kundi la watoto chini ya miaka mitano ambao ulianza kutekelezwa mwaka 2016, umepewa nafasi tena nafasi ya kutekeleza majaribio ya vifo. 

“Tumefanikiwa katika vizazi, sasa hatuna budi kukamilisha hii jozi (pair). Tunanza majaribio kwa ajili ya kugatua majukumu ya usajili wa vifo hapa mkoani Iringa ambapo matokeo yatakayopatikana yatatumika kuboresha mfumo kabla ya kuanza kuenezwa nchi nzima, ” alisema Hudson. 

Kikao hicho pia kilishirikisha wada mbalimabli wakiwemo viongozi wa dini na wanahabari kama sehemu muhimu ya jamii. 

Alifafanua kuwa lengo la kuwashirikisha viongozi dini mbalimbali ni kwa vile vifo vititokea watu wanakimbilia kwenye nyumba za ibada. 

Alisema kuwa viongozi wa dini watawasaidia kutumia fursa walionazo katika kuelimisha wananchi kuhusu umuhimu wa kusajili matukio ya vifo. 

Tofauti na vizazi, kwa mujibu wa takwimu za vifo zaidi ya asilimia 85 vinavyotekea nyumbani wengi huzikwa bila kufika hospitali lakini hao wote huwawanishia kwa viongozi wa dini katika mazishi. 

Hudson aliongeza kuwa wanahabari kama sehemu ya jamii wananafasi kubwa ya kufikisha ujumbe sahihi kwa jamii kuhusu usajili wa vifo, hivyo basi, wanombwa ushirikiano katika mfumo huo wa usajili wa vifo. 

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao hicho cha hamasa aliwapongeza RITA katika mageuzi wanayoendelea kuyatekeleza katika maeneo mbalimbali nchini. 

Alisema kuwa taasisi nyingi zina mengi ya kujifunza hasa katika suala la kusogeza huduma karibu na makazi ya wananchi kwa kugatua madaraka. 

Alisema kuwa kifo ni tukio linalosababisha huzuni kwa sababu hutenganisha na wale tunowapenda ikimanisha hatutaweza kuwa nao tena katika maisha, pamoja hali hiyo, ni muhimu kuandikisha tukio hilo ili kupata cheti cha kifo ambacho kinatumika kama uthibisho wa kisheria wa kifo, aliongeza. 

Masenza alisema kuwa woga wa kifo walionao wananchi unaenda mbele zaidi kusababisha wengi kutosajili matukio ya vifo na kufanya nchi kuwa na wastani wa asilimia 17.5 ya vifo vinavyosajiliwa. 

Alisema kuwa wananchi wanatakiwa kuona uhusiano kati ya kusajili kifo cha ndugu yao na maendeleo ya nchi ili serikali iwezekupanga mipango yake ya maendeleo. 

“Nafahamu zipo nchi ambazo walishaacha kufanya sense kama tunavyofanya kila baada ya miaka kumi na kutumia fedha nyingi kwani nchi hizo wameweka utaratibu ambapo kila mtoto anayezaliwa anasajiliwa na kila mtu anayefariki anasajiliwa hivyo kuwa na takwimu za wananchi wake kila siku,” alsema masenza. 

Aidha, mkuu wa mkoa huyo alitoa rai kwa RITA kutoa fursa ya kuwaeleimisha viongozi wa mikoa umuhimu wa kuandika wosia na kwamba sio uchuro bali ni kwa faida ya familia watakayoiacha mara watakapoondoka duniani. 

Hata hivyo, masenza waliwataka viongozi wa mkoa na wilaya, viongozi wa dini, wanahabari, wadau wa maendeleo na wananchi kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika kutekeleza majario ya mpango wa usajili vifo. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...