Skip to main content

WASICHANA 76 CAMFED WAJIUNGA NA ELIMU YA JUU





Shirika la kuwasaidia watoto wa kike-CAMFED TANZANIA, wilaya ya Iringa limesaidia wasichana 76 kujiunga na elimu ya juu katika vyuo mbalimbali nchini katika kipindi cha mwaka 2017/2018.

Shirika la Camfed linasaidia wasichana kuanzia kidato cha kwanza hadi kidado cha sita na hatimaye kujiunga elimu ya juu kwa wasichana wanaotoka katika familia duni kwa lengo la kuwakwamua na umasikini. 

Mratibu wa miradi ya Camfed Wilaya ya iringa, Abia Mwisaka alisema hayo wakati ya kongamano la wasichana wanaosoma katika vyuo mbalimbali lililoandaliwa na shirika hilo mkoani Iringa jana. 

Alisema kuwa wasichana hao walisaidiwa na shirika hilo kuendelea na elimu ya juu katika vyuo mbalimbali vilivyopo mikoa ya Sumbawanga, Njombe na Iringa. 

Mwisaka alisema kuwa lengo la kongamano hilo lilikuwa kwa ajili kuangalia changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo wasichana walioko vyuoni ili kuona namna gani wanaweza kuepukana nazo. 

Alisema kuwa katika kongamano hilo pia waliwaalika wataalam mbalimbali kwa lengo la kuwasaidia katika Nyanja mbalimbali za maisha pamoja na namna gani wanaweza kuishi wakati wakiwa vyuoni ili kuepukana na hizo changamoto. 

Wataalamu walioalikwa kwenye kongamano ni pamoja na mtaalam wa afya ambaye aliwapitisha katika mambo ya afya kama vile namna ya kujikinga na VVU/UKIMWI, adhari za ndoa za utotoni pamoja na mimba za utotoni. 

Alisema kuwa wasichana wakiwa katika afya njema wataweza kujikinga na kutimiza ndoto zao za kusoma na baadaye kupata ajira kwa vile wasichana wengi wanatoka katika mazingira tofauti, yaani wengine wanatoka maeneo ya vijijini, kwayo wasipopewa elimu ya afya wanaweza kushindwa kutimiza malengo yao. 


Pia, alisema kuwa wasichana hao wakiwa katika kongamano hilo walipitisha katika sera ya ulinzi wa mtoto ili kuwajuza juu ya ulinzi wa mtoto kuhakikisha mtoto analindwa na kuheshimiwa. 

Mwisaka alisema wataalamu wengine walioalikwa ni pamoja na afisa utumishi wa Wilaya ya Iringa aliyewapitisha wasichana hao katika namna ya kuandika CV nzuri, kuandika barua ya kazi na vitu gani wanatakiwa kufanya wanapoitwa kwenye usaili, ili wamalizapo vyuo wasipate shida. 


Mtaalumu mwingine aliyealikwa katika kongamano hilo ni Yule wa bodi ya mikopo kwa wanafunzi ilikuweza kuwaunganisha wasichana hao na bodi ya mikopo ambaye aliwaeleza namna ya kuomba mikopo na nani anastahili kupata mkopo wa wanafunzi. 

Naye, mtaalamu kutoka chuo kikuu kishiriki cha Mkwawa (MUCE) Dr. Winston Mdegella waliwataka wasichana hao waiishi maisha yao na sio maisha ya kufuata mkumbo wanapokuwa vyuoni. 


Alisema kuwa maisha ya chuo ni maisha yanaomwezesha mtu kijitafakari na kujitambua tofuati na maisha ya shule ya msingi na sekondari. 

Dr. Mdegella alisisitiza kuwa maisha ya chuo ni maisha huru lakini uhuru huo usiutumie vibaya ambao mwisho wake unamadhara mengi kuliko faida. 

Aliwaasa wasichana na wanafunzi wengine kusoma kwa bidii kwaani asilimia 80 waielekeze katika masomo na asilimia 20 iliobaki ndio wawezetumia kwa mambo mengine. 



Kwa upande wake, Ofisa Elimu wa Wilaya ya Kilolo, Gloria Kang’omba waliwataka wasichana hao kufikilia nje ya boski kwa kuwa ajira kwa sasa zimekuwa za shida lakini waelekeze mawazo yao katika kujiajiri. 

Alisema kuwa wasichana hao wanatakiwa kusoma kwa bidii liwaweze kufanya vizuri katika masomo yao na hatimaye kukuwa katika soko la ajira. 


Kang’omba alisema kuwa wanafunzi wanaomaliza vyuo nchini ni kubwa na kila mwaka wanafunzi mbalimbali katika vyuo ni wengi kwa hiyo wasichana hao wanabudi kufikilia kujiari kulikokuajiriwa. 



Wakati huohuo, Ofisa mikopo kutoka chuo kikuu kishiriki cha Mkwawa (MUCE) Dr. Kennedy Muhema akitoa taarifa ya bodi ya mikopo wanafunzi alisema kuwa bodi hiyo tangu mwaka 1994/1995 hadi 2017/2018 imeweza kutoa mikopo kwa wanafunzi 438,257 wenye thamani ya trillion tatu (3trn/-). 

Alisema kuwa katika mwaka wa masomo 2017/2018 bodi hiyo imepanga kuwapatia mikopo wanafunzi wapatao 120,417 kati yao 33,857 ni wanafunzi wa mwaka wa kwanza na 86,560 ni wanafunzi wanaoendelea na masomo katika vyuo mbalimbali nchini. 


Dr. Muhema pia alisema kuwa katika mwaka wa masomo 2018/2019 inatajiwa kutoa mikopo kwa wanafunzi wapatao 124,000 ambapo kati yao 40,544 ni wanafunzi wa mwaka wa kwanza. Na Friday Simbaya, Iringa 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...