Skip to main content

POLISI MKOANI IRINGA LIMEWAKAMATA WATU SABA KWA UTAPELI




Na Friday Simbaya, Iringa

Jeshi la Polisi mkoani Iringa limewakamata watu saba wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio mbalimbali mkoani hapa kwa kukamatwa na vitu mbalimbali zikiwemo noti bandia dola za kimarekani pamoja na madini bandia.

Akizungumza na wanahabari mjini Iringa leo kamanda wa polisi mkoa wa Iringa ACP Juma Bwire Makanya alisema kuwa wamemkamata mtuhumiwa Emmanuel Mtweve , 41, mfanyabiashara mkazi wa Tabata wa jijini Dar es Salaamu akiwa na noti bandia 63 mfano wa dola za kimarekani.

ACP Bwire alisema mtuhumiwa huyo Mtweve pia alikamatwa akiwa na madini bandia mithili ya dhahabu yenye uzito wa kilogramu 3.5 baada ya kufanyia upekuzi ndani ya gari yake keneye namba za usajili T 419 DLL aina ya Brevis.

Alisema kuwa katika swala la ufuatiliaji wamekamata wahusika wengine wanatuhumiwa kujihusisha na matukio mbalimbali akiwemo Abdallah Mohamed,43, mkulima na mkazi wa Madoto Mburahati, Abukakari Mwamedi, 40, mkazi wa Mbarali Mbeya, Seif Seleman,37, mkazi wa Chanika, Christopher Mgie, 37, Frank Lutanile na Abuu Mbinga wote wakazi wa Itamba Mbarali, mkoani Mbeya.

Vitu mbalimbali walivyokamatwa navyo ni mabunda matano ya makaratasi ya mfano wa fedha, sanduku la kienyeji la kubebea vitu hivyo, simu 19 za aina mbalimali za kuwapigia kwa ajili ya kutapeli, hirizi tano, rubber band za kufungia noti bandia na kilo nne za madini bandia mithili za dhahabu.

Aidha, jeshi la polisi limetoa wito kwa wananchi kuwa makini na kutokaa taarifa juu ya watu wa aina hiyo.

Katika hatua nyingine, jeshi la polisi mkoani Iringa linawatafuta watu sita (6) wanaosidikikiwa ni majambazi kwa kuvamia Fuad Faraji Abri,25, mkazi wa Wilolesi manispaa ya Iringa na kmpiga risasi kwenye paja la mguu wa kushoto.

ACP Bwire alisema kuwa tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 13/07/2018 katikamaeneo ya Wilolesi Kata ya Gangilonga Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa.

Alisema kuwa majabazi hao alimvamia nyumbani kwake na watu siata walijificha nyuso zao kwa vikoi vya kimasai ambao waliruka uzio wa nyumba kwa kutumia ngazi mbili na kumteka mlinzi kwa kumfunga kamba mikononi kisha kuvunja mlango wa nyumba kwa nia kupora mali.

Kamanda Bwire alifafanua kuwa majabazi hao walifyatua risasi mbili za bastola ambazo zilimujeruhi Abri kwenye paja la mguu wa kushoto kitendo kilicholeta majibizano ya risasi pande mbili na kupelekea majambazi kukimbia kutoka eneo la tukio.

Hata hivyo, watuhumiwa wawili wamekamatwa kufuatia tukio hilo la kunyang’anya kwa kutumia silaha na msako bado unaendelea.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...