Skip to main content

ASILIMIA 42 YA WATOTO CHINI YA MIKA MITANO MKOANI IRINGA WAMEDUMAA



Kikundi cha wazee wa Kilolo cha utamaduni wa kabila la wahehe kikitoa burudani wakati wa Kilele cha maadhimisho unyonyeshaji maziwa ya mama duniani yalioanza tarehe 01-07, August, 2018 yaliofanyika kimkoa katika Kijiji cha Kilolo wilayani Kilolo, mkoani Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)






Takwimu zinaonesha kuwa asilimia 42 ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano mkoani Iringa wamedumaa, asilimia 3.6 wamekonda na asilimia 13.8 wana uzito pungufu ukilinganisha na umri wao. 

Akizungumza na mganga mkuu wa mkoa wa iringa (RMO), Dr. Robert Salim kwa nia ya Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi wakati wa siku ya killele cha maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji wa maziwaya mama duniani yaliyofanyika kimkoa katika kijii cha Kilolo wilayani Kilolo, mkoani iringa jana. 

Alisema kuwa unyonyeshaji watoto maziwa ya mama unafaida nyinyi kwa upande zote mbili kwa mtoto anayenyonya maziwa na mama anayenyonyesha. 

Hapi alisema kuwa kwa mtoto anayenyonya maziwa ya mama ndiyo chakula pekee kinachompatia virutubishi vyote anavyohitaji kwa uwiano sahihi kwa afya na ustawi. 

Aliongeza kuwa maziwa ya mama ndiyo chakula pekee chenye viini vya kingamwili ambavyo hufanya kazi kama chanjo inayomlinda mtoto dhidi ya maradhi na kumsaidia kuhimili maradhipindi anapopata maambulizi mbalimbali. 

Hapi alisema kuwa faida nyingine ni kwamba maziwa hayo ya mama humeng’enywe na kufyonzwa kwa urahisi zaidi mwa mtoto ukilinganisha na vyakula akue na apate maendeleo mazuri kimwili na kiakili. 

“Mtoto anayenyonyeshwa ipasavyo huongezaka urefu kulingana na umri kwa kasi nzuri hali inayomfanya awe na kiwango kizuri cha uelewa wa mambo yanayomzunguka,” alisisitiza. 

Alisema kuwa hali hii huchangia kupata alama nzuri katika masoso yake darasani na kuongeza kuwa unyonyenyeshaji wa maziwa ya mama unaupatia nguvu mfumo wa ukuaji na maendeleo ya ufahamu na utambuzi (IQ)wa mtoto. 

Hivyo, kwa kiasi kikubwa husaidia katika kuimarisha mannikio ya elimu, ushirika katika nguvu kazi na kuongeza kipato katika maisha ya baadaye ya mtoto. Na Friday Simbaya, Kilolo 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...