Skip to main content

HALMASHAURI YA MUFINDI IMEANZA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA VIJIJINI




Diwani wa VitiMaalum Tarafa ya Kasanga kutoka Mninga katika Kijiji cha Mkalala, Asumpta Adriano Mtende akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi hivi karibuni. (Picha na Friday Simbaya)
`


Na Friday Simbaya, Mufindi 

Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa imeanza kuboresha huduma za afya vijijini kwa kukatarabati na kujenga miundombinu muhimu katika vituo vyake mbalimbali vya afya ili kusogeza huduma hizo karibu na wananachi. 

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi Festo Elia Mgina hivi karibuni watika wa Kikao cha Baraza la Madiwani cha mwaka, ambapo pamoja na mambo mengine kikao hicho kilipitia taarifa ya utekeleazji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2017/2018. 

Mkutano huo wa Baraza la Madiwani ulikuwa na agenda ya uchaguzi wa makamu mwenyekiti wa halmashauri ambapo Diwani wa Kata ya Sadani, Ashery Mtono alichaguliwa kuwa makamu mweneyekiti mpya wa halmashauri hiyo pamoja na uundwaji upya wa kamati za kudumu za halmashauri. 

Alisema kuwa halmashauri hiyo imeanza kuboresha utoaji wa huduma za afya vijijini kwa kuboresha vituo vya afya ili kusogeza huduma hizo karibu na wananchi kwa kuzingatia kuwa halmashauri hiyo haina hospitali ya wilaya. 

Mgina alisema kuwa halmashauri hiyo haina hospitali ya wilaya baada ya Wilaya ya Mufindi kuganyika na kuzaliwa kwa Halmashauri ya Mji Mafinga na Hospitali ya Mafinga ya Wilaya kuwa chini ya halmashauri hiyo mpya. 

Alisema kuwa awali, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ilikuwa inatumia Hospitali ya Mafinga kama hospitali yake ya wilaya lakini kutokanana mgawanyiko huo kwa sasa ipo chini Halmashauri ya Mji Mafinga. 

Alifafanua kuwa ili kusongeza huduma za afya karibu na wanannchi na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Mafinga, halmashauri hiyo imeanza kukarabati na kujenga miundombinu muhimu katika vituo mbalimbali vya afya. 

Mgina alisema kuwa katika Kituo cha Afya cha Malangali wamejenga jengo la akina mama la kujifungulia, maabara pamoja na nyumba ya mtumishi. 

Aidha, katika kituo kingine cha Afya cha Ifwagi pia wamekarabati na kujenga miundombinu muhimu hususan jengo la upasuaji, jengo la akina mama kujifungulia, maabara na nyumba ya mtumishi kwa kushirikiana na serikali kuu pamoja na wadau wa maendeleo mbalimbali. 

Aliongeza kuwa kupitia mpango wa ‘force account’, serikali kuu imetoa shilingi milioni 400 (400,000,000/-) kwa kila kituo cha afya yaani Malangali na Ifwagi kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu muhimu. 

Katika upande wa mapato, mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi alisema kuwa halmashauri imekusanya zaidi ya asilimia 90 ya mapato yake ya ndani katika kipindi cha mwaka 20172018, ambao ni mwaka wa fedha ulioisha ijumaa wiki iliyopita. 

Alisema kuwa halmashauri hiyo ilijewekea malengo ya kukusanya mapato ya ndani ya shilingi bilioni 3.8 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na kufanyikwa kukusnaya zaidi ya asilimia 90. 

Mgina alifafanua kuwa asilimia kubwa ya mapato yake ya ndani yanategemea kutoka mazao ya misitu zikiwemo mbao na mirunda kwa zaidi ya asilimia 75 yanatokanayo na mazao mbalimbali ya misiti. 

Alisema kuwa kumekuwepo na changamoto katika kukusanya mapato kutokana zikiwemo utoroshaji wa mbao kwa lengo kukwepa kulipa usharu kwa baadhi ya wafanyabiashara pamoja na kuwepo kwa miundombinu ya barabara sio rafiki. 

Alisema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya utoroshaji wa mazao ya misitu halmashauri hiyo imefungua mageti mengi katika maeneo mbalimbali kwa ajili ya kudhibiti utoroshaji pamoja na kuimarisha doria za usiku na mchana kwa kushirikiana na wataalamu ya halmashauri hiyo. 

Wakati huohuo, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, mkoani iringa imetumia zaidi ya shilingi milioni 39 katika utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira chini ya program ya maji vijijini (RWSSP) kwa mwaka wa fedha 2017/2018 kupitia mapato yake ya ndani. 

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo Ijumaa wiki iliyopita, John Bosco Quman kwa niaba ya mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Mufindi wakati Kikao cha Baraza la Madiwani cha Mwaka alisema kuwa jumla ya visima vibovu vya maji 21 vilikarabatiwa kupitia program maji vijijini. 

Alisema kuwa kuwa halmashauri hiyo imekarabati visima vya maji katika vijiji vya Ihanzutwa, Kihanga, Nzivi na Ibatu kupitia mpango wa payment by result (PbR) na kufafanua kuwa katika kijiji cha Kihanga visima nane (8) vilikarabitwa, Ihanzutwa visima vinne (4), Nzivi visima vitano (5) na Ibatu visima vinne (4) vilitengenezwa na vinatoa huduma. 

Quman alisema alifafanua kuwa ukarabati wa visima vya maji 21 katika vijiji hivyo uligharimu jumla ya shilingi 13,650,000/- kupitia program ya maji vijijini (RWSSP) chini ya mpango wa payment by result. 

Alisema kuwa miradi mimgine iliyotekelezwa katika mwaka wa fedha 2017/2018 chini ya RWSSP ni pamoja na ukarabati wa mtego wa maji wa mradi wa Kijiji cha Ikimilinzowo uliogharami zaidi ya shilingi milioni 12, utekelezaji wa shughuli za kampeni ya usafi wa mazingira shilingi milioni 7.3 na usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ya maji shilinhi milioni sita (6) mtawaliwa (respectively). 









Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...