Skip to main content

WATOTO WAITAKA SERIKALI KUTUNGA SHERIA KALI ...



Na Friday Simbaya, Mufindi 

Wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wilayani Mufindi mkoani Iringa wameiomba serikali kwa kushirikiana na wadau wa haki za watoto kutunga sheria kali dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyochangia watoto kushindwa kutimiza ndoto zao. 

Wakizungumza jana wakati wa semina wa mabaraza ya watoto ngazi ya kata wanafunzi hao wanasema vitendo vya ukatili vimekuwa vikiongezeka kila siku kwa jamii inayo wazunguka kutokana na kutokuwapo kwa sheria kali dhidi yao huku wazazi wakionekana kushindwa kutimiza haki za watoto. 

Malezi mabaya ya familia yanachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa vitendo viovu ikiwamo ubakaji na ulawiti hivyo Wazazi ,walezi na jamii kwa ujumla wanayonafasi kubwa ya kuijenga jamii yenye maadili dhidi ya vitendo viovu. 

Jumla ya watoto 140 kutoka kata za Bumilinyinga, Idunda na Ihowanza walishirika semina ya baraza la watoto ngazi ya kata kuhusu ukatili wa kijinsia iliyoandaliwa na Asasi isiyoyakiserikali ya SOS Children’s Villages Tanzania kwa shirikiana na Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa. 

Mmoja wa wajumbe wa baraza la watoto toka kata ya Ihowanza, Evelina Mwilapwa ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari Ihowanza alisema kuwa serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inapaswa kutunga sheria kali itakayoza kudhibiti viovu dhidi ya watoto. 

Alisema kuwa serikali kuwa serikali inatakiwa kulitilia umuhimu suala la ukatili wa kijinsia hasa kwa watoto wa kike ambao wana kumbana nalo kuanzia ngazi ya familia hadi jamii. 

Mwilapwa alisema kuwa wapo wazazi na walezi wenye mtazamo hasa juu ya watoto wakike kwa kuwanyimwa fursa ya kupata elimu pamoja na kubaguliwa. 

Ofisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi Navoneiwa Mfinanga alisema licha ya kutoa elimu kwa wazazi bado changamoto ya ukatili kwa watoto imeonekana kukithiri miongoni mwa wazazi na walezi huku akieleza mikakati ya serikali juu ya jambo hilo. 

Alisema kuwa changamoto za ukatili wa kijinsia umeanza kupungua kutokana na elimu ya ukatili wa kijinsia kwa jamii kupitia kamati mbalimbali mazingira hatarishi. 

Mfinanga alisema kuwa yeye kama mratibu wa mabaraza ya watoto wamefanyikiwa kuunga mabaraza ya watoto ngazi ya kijiji,kata na ngazi ya wilaya. 

Aidha, ofisa maendeleo ya jamii aliyeshiriki kuendesha semina kwa watoto wa mabaraza ya watoto ngazi ya kati ni Grace Kalomeji toka halmashuri ya mji mafinga, wilayani Mufindi. 

Kokutona Kayungi ni Ofisa Mradi wa Shirika la SOS Children’s Villages Tanzania wilayani Mufindi kupitia mradi wa kuwezesha wanawake kiuchumi na haki za watoto alisema kuwa semina hiyo walikuwa ni kuimarisha na kuyajengea uwezo mabaraza ya watoto ili wawezekutambua haki zao ili waweze kupaza sauti zao juu ya masuala ya ukatili wa kijisia. 

Alisema kuwa kupitia mabaraza ya watoto ni jukwaa la watoto ambapo wanajadili mambo yao yanayowahusu wao wenyewe hasa ubakaji, mimba za utotoni pamoja na wawake kutopewa haki ya kumiliki mali. 

kayungi pia alisema ukalitili ya kijinsia mara nyingi utokea katika ngazi ya familia kwa kupitia mabaraza hayowa watoto wanafundishwa namna ya kutambua haki za ilikuweza kuripoti vitendo vya ukatili katika madawati ya kijinsia ambayo hapo katika maeneo yao. 

Aliongeza kuwa Asasi ya SOS childrens Villages Tanzania pia inatoa mafunzo ya kujenga uwezo wa walezi wa watoto, familia zao na jamii ili watoto wapate malezi ya kutosha. 

Kayungi alisema kuwa watoto takribani 140 toka kata za Bumilinyinga, Idunda na Ihowanza wamekutana kupitia mabaraza ya watoto yaliyopo Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa kubadilishana mitazamo na kupaza sauti kwa mambo yanayowahusu. 

“Watoto hawa kwa sasa wanakabiliwa na changamoto nyingi za vitendo vya ukatili kama kubakwa, ndoa za utotoni pamoja na kufanyishwa kazi ngumu na katika siku za hivi karibuni,” alisema. 



Mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...