Skip to main content

 IRINGA WAANZA MAANDALIZI YA MPANGO MKAKATI WA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA



 

Iringa. Katika juhudi za kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia (GBV), Mkoa wa Iringa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali umeanza kuandaa rasimu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake, Watoto na Wanaume (MTAKUWA II) ngazi ya mkoa, kwa lengo la kuhakikisha ukatili unatokomezwa kwa kiwango cha juu kabisa.

 

Kikao kazi cha maandalizi ya mpango huo wa kitaifa wa miaka mitano (MTAKUWA II 2024/25 – 2028/29), kiliongozwa jana na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Saida Mgeni, ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Maendeleo ya Jamii mkoani humo.

 

Afisa Maendeleo ya Jamii na Mratibu wa MTAKUWA/NPA-VAWC mkoa wa Iringa, Grace Simalenga, alisema mpango mkakati wa awamu ya pili umejumuisha pia wanaume na wavulana ili kuhakikisha mapambano dhidi ya ukatili yanagusa makundi yote.

 

“Leo tumekutana kupitia maandalizi ya mpango mkakati wa mkoa kwa ajili ya kupambana na ukatili dhidi ya wanawake, watoto, wanaume na wavulana. Tulihusisha waratibu wa halmashauri, viongozi wa dini, taasisi mbalimbali, pamoja na waandishi wa habari ili kuhakikisha mpango huu unatekelezeka kwa ufanisi,” alisema Simalenga.

Aliongeza kuwa kikao hicho kimewezeshwa na Shirika la SOS Children’s Villages kupitia ushirikiano wa serikali na sekta binafsi (PPP). Shirika hilo limekuwa mstari wa mbele katika kupinga mimba za utotoni na kuwawezesha wasichana waliojaliwa watoto wakiwa katika umri mdogo.

 

Meneja Miradi wa SOS Mkoa wa Iringa, Victor Mwaipungu, alisema shirika hilo limeamua kuunga mkono juhudi za serikali kwa kujenga uwezo wa kamati za MTAKUWA II kuanzia ngazi ya mkoa, halmashauri hadi kata.

 

“Kamati hizi zikijengewa uwezo na uelewa wa kutosha kuhusu maeneo ya kipaumbele ya MTAKUWA II, mapambano dhidi ya ukatili yatakuwa rahisi na yenye tija,” alisema Mwaipungu.

 

Kwa upande wake, Mchungaji Upendo Koko kutoka KKKT Dayosisi ya Iringa, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Idara ya Wanawake na Jinsia kwa Jumuiya ya Makanisa ya Kikristo Tanzania mkoani Iringa, alisema rasimu hiyo ikikamilika itasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa vitendo vya ukatili katika jamii.

 

Naye Mrakibu Msaidizi wa Polisi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto mkoani Iringa, Elizabeth Swai, alisema jukumu kubwa la wajumbe wa kamati hiyo ni kutoa elimu na kuhakikisha makosa yote yanayohusiana na ukatili wa kijinsia yanashughulikiwa ipasavyo.

 

Aidha, Afisa Ustawi wa Jamii na Mratibu Mwenza wa MTAKUWA II mkoa wa Iringa, Martin Chuwa, alisema mpango mkakati wa awamu ya pili umeboreshwa kwa kuongeza maeneo mapya, ikiwemo ukatili wa kimtandao na kuhusisha zaidi wanaume na wavulana.

“Takwimu zinaonesha kuwa ukatili dhidi ya wanaume nao unaongezeka mwaka hadi mwaka. Pia mpango huu umeongeza ushirikiano wa taasisi binafsi katika nafasi za uratibu,” alisema Chuwa.

 

MTAKUWA wa awamu ya kwanza ulikamilika, na sasa awamu ya pili (MTAKUWA II) inaanza kutekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano, 2024/25 – 2028/29, kwa lengo la kuhakikisha Tanzania inakuwa taifa lisilo na ukatili wa kijinsia.

Mwisho










Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...