Skip to main content

Mgombea Ubunge Kalenga Aomba Ridhaa ya Wananchi, Aahidi Kuboresha Huduma za Afya




Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kumpa tena ridhaa ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM wakati wa kampeni, mgombea huyo alisema kipindi cha miaka mitano iliyopita kilikuwa cha kujifunza, huku akieleza kuwa endapo atapewa nafasi nyingine, ataendeleza miradi ya maendeleo aliyoianzisha.

Alibainisha kuwa moja ya changamoto zinazowakabili wananchi ni ukosefu wa vyumba vya kuhifadhi maiti katika vituo vya afya, na kuahidi kushirikiana na Serikali kuhakikisha kila kituo kinakuwa na huduma hiyo ili kupunguza gharama za kupeleka maiti katika Hospitali ya Tosamaganga.

Aidha, alitaja mafanikio aliyoyapata katika kipindi chake cha ubunge ikiwemo kufanikisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mgama, hatua ambayo imesaidia kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma muhimu.

“Chama Cha Mapinduzi ndicho chama pekee chenye uwezo wa kudumisha amani na usalama wa nchi hii. Tuendelee kukiamini na kukipa kura zetu ili maendeleo yawe endelevu,” alisema.

 


Iringa. Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kalenga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ameomba wananchi wa kata ya Lyamgungwe, Wilaya ya Iringa, kumpa tena ridhaa ya kuendelea kulitumikia jimbo hilo katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu.

Akizungumza na wananchi na wanachama wa CCM wakati wa kampeni, mgombea huyo alisema kipindi cha miaka mitano iliyopita kilikuwa cha kujifunza, huku akieleza kuwa endapo atapewa nafasi nyingine, ataendeleza miradi ya maendeleo aliyoianzisha.

Alibainisha kuwa moja ya changamoto zinazowakabili wananchi ni ukosefu wa vyumba vya kuhifadhi maiti katika vituo vya afya, na kuahidi kushirikiana na Serikali kuhakikisha kila kituo kinakuwa na huduma hiyo ili kupunguza gharama za kupeleka maiti katika Hospitali ya Tosamaganga.

Aidha, alitaja mafanikio aliyoyapata katika kipindi chake cha ubunge ikiwemo kufanikisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mgama, hatua ambayo imesaidia kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma muhimu.

“Chama Cha Mapinduzi ndicho chama pekee chenye uwezo wa kudumisha amani na usalama wa nchi hii. Tuendelee kukiamini na kukipa kura zetu ili maendeleo yawe endelevu,” alisema.

 



 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...