Songwe. Zaidi ya wananchi 500 wanatarajiwa kufikiwa na huduma za matibabu ya macho pamoja na afya ya kinywa na meno kupitia kambi maalum ya matibabu ya siku tano iliyoanzishwa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kusogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Juma Ramadhani, amesema kambi hiyo imelenga kuwahudumia wananchi, hususan wanaoishi maeneo ya vijijini, ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya umbali, gharama kubwa za matibabu pamoja na uhaba wa wataalamu wa afya ya kibingwa.
Akizungumza na The Citizen leo Januari 27, 2026, Dk Ramadhani amesema katika kipindi cha siku tano, hospitali inatoa huduma za uchunguzi wa macho, matibabu ya magonjwa mbalimbali ya macho, ushauri wa kitaalamu pamoja na huduma za uchunguzi na matibabu ya kinywa na meno kwa gharama nafuu au bure, kulingana na hali ya mgonjwa.
“Tumeona ongezeko la magonjwa ya macho na matatizo ya meno katika jamii, hivyo tumeamua kusogeza huduma hizi karibu na wananchi ili waweze kupata matibabu mapema na kuepuka madhara makubwa baadaye,” amesema Dk Ramadhani.
Ameeleza kuwa kambi hiyo inaendeshwa na madaktari bingwa watatu wa macho na afya ya kinywa na meno kutoka hospitali hiyo, wakitoa huduma za upimaji wa macho, upasuaji wa macho, uchunguzi wa meno pamoja na upasuaji mdogo wa meno.
“Tumeona wananchi wengi hawajui kuwa matatizo yao mengi yanaweza kutibiwa hapa hapa Songwe. Hakuna sababu ya kwenda nje ya mkoa ilhali Mkoa wa Songwe una Hospitali ya Rufaa yenye wataalamu bingwa na vifaa vya kisasa kwa gharama nafuu,” ameongeza.
Kwa upande wake, Ofisa Habari na Mahusiano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe, Robert Hussein, amesema kambi hiyo imelenga kuwahudumia wananchi wasiopungua 500, huku hospitali ikiwa na uwezo wa kuhudumia zaidi ya wagonjwa 100 kwa siku.
Ametoa wito kwa wananchi kujenga utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara (check-up) ili kugundua magonjwa mapema na kupunguza gharama za matibabu.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kupata huduma wameipongeza hospitali kwa hatua hiyo wakisema imepunguza gharama za kusafiri umbali mrefu na kuwapa fursa ya kupata huduma za kibingwa ambazo hapo awali zilikuwa ngumu kufikiwa.
Serikali ya Mkoa wa Songwe imesema itaendelea kushirikiana na hospitali pamoja na wadau wa afya kuhakikisha huduma za kibingwa zinaendelea kusogezwa karibu na wananchi kwa lengo la kuboresha afya ya jamii na kuongeza tija katika shughuli za maendeleo.
“Tumeona ongezeko la magonjwa ya
macho na matatizo ya meno katika jamii, hivyo tumeamua kusogeza huduma hizi
karibu na wananchi ili waweze kupata matibabu mapema na kuepuka madhara makubwa
baadaye,” amesema.
Ameeleza kuwa kambi hiyo
inaendeshwa na madaktari bingwa watatu wa macho na afya ya kinywa na
meno kutoka hospitali hiyo, wakitoa huduma za upimaji wa macho, upasuaji wa
macho, uchunguzi wa meno pamoja na upasuaji mdogo wa meno.
“Tumeona wananchi wengi hawajui
kuwa matatizo yao mengi yanaweza kutibiwa hapa hapa Songwe. Hakuna sababu ya
kwenda nje ya mkoa ilhali tuna Hospitali ya Rufaa yenye wataalamu na vifaa vya
kisasa kwa gharama nafuu,” ameongeza Dk Ramadhani.
Kwa upande wake, Ofisa Habari
na Mahusiano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe, Robert Hussein,
amesema kambi hiyo imelenga kuwahudumia wananchi wasiopungua 500, huku
uwezo wa kuhudumia wagonjwa zaidi ya 100 kwa siku ukiwepo.
Ametoa wito kwa wananchi kujenga
utamaduni wa kufanya uchunguzi wa afya mara kwa mara (check-up) ili
kugundua magonjwa mapema na kupunguza gharama za matibabu.
Baadhi ya wananchi waliojitokeza
kupata huduma wameipongeza hospitali kwa hatua hiyo wakisema imepunguza gharama
za kusafiri umbali mrefu na kuwapa fursa ya kupata huduma za kibingwa ambazo
awali zilikuwa ngumu kufikiwa.
Serikali ya Mkoa wa Songwe
imesema itaendelea kushirikiana na hospitali pamoja na wadau wa afya
kuhakikisha huduma za kibingwa zinaendelea kusogezwa karibu na wananchi kwa
lengo la kuboresha afya ya jamii na kuongeza tija katika shughuli za maendeleo.



Comments