Skip to main content

Baraza la Madiwani Mafinga Lapitisha Bajeti ya Sh38.6 Bilioni kwa 2026/27


Mafinga. Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Mji Mafinga limepitisha rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2026/2027 yenye jumla ya Sh38,651,155,000, katika kikao kilichofanyika Februari 21, 2026, kikilenga kuimarisha huduma za kijamii na kuchochea maendeleo ya mji huo.

Akiwasilisha rasimu hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Afisa Mipango na Uratibu wa Mji, Peter Ngusa, alisema halmashauri imejipanga kukusanya na kutumia fedha hizo katika utekelezaji wa majukumu ya msingi, miradi ya maendeleo na kuboresha ustawi wa wananchi.

Alifafanua kuwa kati ya fedha hizo, Sh8,844,800,000 zinatarajiwa kukusanywa kutoka mapato ya ndani, Sh942,454,000 ni ruzuku ya matumizi mengineyo (OC), Sh23,376,336,000 ni ruzuku ya mishahara, na Sh5,487,565,000 ni ruzuku kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Kwa mujibu wa mpango huo, vipaumbele vilivyowekwa ni pamoja na kupanua wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, kununua maeneo kwa ajili ya uwekezaji, kuendeleza shamba la parachichi la Makalala, kuimarisha miradi ya kimkakati, kuboresha huduma za jamii na kuimarisha usafi pamoja na uhifadhi wa mazingira.


Kikao hicho kilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Linda Selekwa, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Fidelica Myovela, Mwenyekiti wa Halmashauri, Regnant Kivinge, Mbunge wa Viti Maalum – Vijana kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jasmine Ng’umbi, pamoja na Mbunge wa Jimbo la Mafinga Mjini, Dickson Lutevelle maarufu kama ‘Villa’.

Mikopo ya Asilimia 10 Yapewa Kipaumbele

Akichangia hoja ya bajeti, Ng’umbi alimuomba Mkurugenzi kuhakikisha mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu inatolewa bila urasimu na ucheleweshaji usio wa lazima.

Alisema kumekuwapo malalamiko kutoka kwa vikundi vinavyoomba mikopo hiyo lakini kucheleweshewa au kunyimwa bila sababu za msingi, hali inayokwamisha jitihada za kuwawezesha wananchi kiuchumi.

“Mikopo hii ni haki ya makundi maalumu kwa mujibu wa sheria na miongozo ya Serikali, hivyo ni muhimu kuweka utaratibu wazi na wa haki,” alisisitiza Ng’umbi.


Kwa upande wake, Lutevelle aliwataka vijana wanaofanya shughuli katika Stendi ya Mabasi Mafinga kuimarisha umoja na kujiunga katika vikundi vinavyotambulika ili waweze kunufaika na mikopo, mafunzo na mitaji kupitia mipango ya uwezeshaji.

Katika kuonesha dhamira ya kuwaunga mkono, wabunge hao walichangia jumla ya Sh700,000 taslimu kusaidia vikundi vya vijana vinavyofanya shughuli katika eneo hilo.

Changamoto ya Maji Yatajwa

Wakati huohuo, wajumbe wa Baraza la Madiwani walieleza changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama, wakibainisha kuwa ni asilimia 68 tu ya wakazi wa Mafinga wanaopata huduma hiyo kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mafinga (MUWASA).

Wameiomba Serikali kuharakisha utekelezaji wa mradi wa maji wenye thamani ya Sh48 bilioni unaoendelea, ili kuongeza wigo wa huduma na kufikia wananchi wengi zaidi.

Baada ya majadiliano ya kina, Baraza la Madiwani lilipitisha rasmi bajeti hiyo na kuahidi kusimamia kwa karibu utekelezaji wake ili kuhakikisha inaleta matokeo chanya kwa wananchi wa Mafinga.
















 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...