Skip to main content

Mawelewele Yafuta Daraja la Sifuri kwa Miaka Miwili Mfululizo


Iringa. Shule ya Sekondari Mawelewele iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imeandika historia mpya kwa kufuta daraja la sifuri kwa miaka miwili mfululizo katika matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne kwa shule za serikali. Hatua hiyo imetajwa kuwa mafanikio makubwa katika kuinua kiwango cha ufaulu na hadhi ya shule hiyo kitaaluma.

Kutokana na matokeo hayo, shule imefanikiwa kushika nafasi ya pili ngazi ya halmashauri, ikiendelea kuonesha mwelekeo chanya wa kitaaluma na ushindani bora miongoni mwa shule za sekondari za manispaa hiyo.

Mkuu wa shule hiyo, Mwl. Robert Ngimba, amesema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya walimu, wanafunzi na wazazi, pamoja na kuimarika kwa nidhamu, ufuatiliaji wa maendeleo ya wanafunzi na utoaji wa masomo ya ziada kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum.

Ameeleza kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 1998 na hadi sasa imekuwa na wakuu wa shule wanne waliomtangulia, yeye akiwa wa tano.

“Shule yetu inaendelea kukua kitaaluma. Mwaka 2024 tulifanikiwa kufaulisha wanafunzi wote na kufuta daraja la sifuri katika mitihani ya taifa ya Kidato cha Nne. Mwaka 2025 pia wanafunzi wote 150 waliofanya mtihani walifaulu, hivyo kuendelea kufuta daraja la sifuri kwa mwaka wa pili mfululizo,” amesema Mwl. Ngimba.

Aidha, shule hiyo imeongeza ufaulu bora (Division I–III) hadi kufikia asilimia 65, hatua inayoonesha kuimarika kwa ubora wa matokeo. Katika ngazi ya halmashauri kwa shule za serikali, Mawelewele imeshika nafasi ya pili ikitanguliwa na Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Iringa.

Katika ngazi ya mkoa, kati ya jumla ya shule 154, ni shule 12 pekee zilizopata tuzo ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, na Mawelewele ikiwa miongoni mwa shule hizo 12 bora.

Akizungumzia siri ya mafanikio hayo, Ngimba amesema ni kujituma kwa watumishi, kuwa na lengo la pamoja, usimamizi madhubuti na walimu kujitoa kwa hali na mali kuhakikisha wanafunzi wanafundishwa kwa ubora, sambamba na ushirikiano mzuri kati ya shule, wazazi na wanafunzi.

Ametoa shukrani za pekee kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha za elimu bila malipo, ambazo zimesaidia kutatua changamoto mbalimbali shuleni hapo. Pia, utaratibu wa wanafunzi kupata chakula cha mchana umeongeza muda wa kujisomea na kuimarisha umakini darasani.

Wadau wa elimu wamesema mafanikio hayo ni ishara kuwa mikakati iliyowekwa imeanza kuzaa matunda, huku wakisisitiza umuhimu wa kuendeleza ari hiyo ili shule iweze kushika nafasi ya juu zaidi katika matokeo yajayo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...