Skip to main content

MBUNGE KIHENZILE AZINDUA KITUO CHA AFYA MAKUNGU CHA SH MILIONI 500


Mufindi. MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kusini, David Kihenzile, amezindua Kituo cha Afya cha Makungu kilichojengwa kwa gharama ya Sh milioni 500 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, hatua inayotarajiwa kumaliza changamoto ya upatikanaji wa huduma za afya kwa zaidi ya wananchi 17,000 wa kata hiyo na maeneo ya jirani.


Kukamilika kwa mradi huo kunatajwa kuwa sehemu ya utekelezaji wa ahadi za Rais Samia Suluhu Hassan ndani ya siku 100 za mwanzo wa muhula wake mpya wa uongozi baada ya Uchaguzi Mkuu, ambapo Serikali imeendelea kuimarisha miundombinu ya afya na kusogeza huduma karibu na wananchi.

Akizungumza leo Februari 23, 2026, wakati wa ziara yake ya siku nne jimboni humo, Mbunge Kihenzile ambaye pia ni Naibu Waziri wa Uchukuzi, alisema ujenzi wa kituo hicho ni mkombozi mkubwa kwa wakazi wa Makungu, Mgololo na maeneo ya jirani waliokuwa wakilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya, hususan huduma za mama na mtoto.

Alisema kipindi cha mvua wananchi wa ukanda wa Mgololo wamekuwa wakikumbana na adha kubwa kutokana na miundombinu kuwa hafifu, hali iliyosababisha baadhi yao kushindwa kufika hospitali kwa wakati.


“Kipekee tunamshukuru sana Rais Dk. Samia Suluhu Hassan. Tulimfikishia ombi maalumu kuwa Makungu ni kata muhimu, na Mgololo ni ukanda ambao wakati wa mvua wananchi hupata tabu kubwa; wapo waliokuwa wanapoteza maisha kwa kukosa huduma za afya kwa wakati. Leo tunajivunia kuwa na kituo cha afya kitakachohudumia Makungu pamoja na maeneo ya Idete na Kiohela,” alisema Kihenzile.

Wananchi waliohudhuria hafla ya uzinduzi walieleza kuwa kituo hicho kitapunguza gharama za usafiri, kuokoa muda na kuongeza upatikanaji wa huduma za dharura, jambo litakalochochea maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika eneo hilo.

 
















 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...