Skip to main content

Mahakama Kuu Yamuhukumu Kifo Baba Aliyemuua Mtoto Wake kwa Imani za Utajiri


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Iringa imemhukumu kunyongwa hadi kufa, Joseph Muhulila (28), mkazi wa Mtaa wa Lukosi, Kata ya Mkwawa, Manispaa ya Iringa, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi mtoto wake wa kumzaa, Timothy Muhulila (miaka 4), akidaiwa kufanya hivyo kwa imani za kujipatia utajiri.

Hukumu hiyo iliyosomwa kwa zaidi ya saa nne imetolewa na Jaji Angaza Mwipopo katika kesi namba 25532 ya mwaka 2025, akieleza kuwa ushahidi uliowasilishwa mahakamani umethibitisha bila kuacha shaka kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume cha vifungu vya 196 na 197 vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya mwaka 2022.

Upande wa Jamhuri uliwakilishwa na mawakili David Mwakiborwa na Jackson Mwakalinga.

Kwa mujibu wa mahakama, tukio hilo la kikatili lilitokea Aprili 12, 2025, ambapo mshtakiwa alimuua mtoto wake kisha kumkatakata vipande vidogo na kuvitupa kwenye shimo la choo.

Akisoma maelezo ya ushahidi, Jaji Mwipopo alinukuliwa akisema:

“Mtuhumiwa alikiri kukata mwili wa marehemu vipande vidogo na kuviponda mifupa kwa jiwe kubwa kabla ya kuvitupa kwenye shimo la choo.”

Baada ya kukamatwa kwa mtuhumiwa, mabaki ya mwili yalipatikana katika tenki la maji taka na kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu wa vinasaba (DNA), ambapo majibu yalionesha kwa asilimia 99 kuwa yalihusiana na marehemu.

Mahakama ilieleza kuwa upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi 13, ambao ushahidi wao uliisaidia kufikia uamuzi wa kumtia hatiani mshtakiwa na hatimaye kumhukumu adhabu ya kifo.



Hata hivyo, wakili wa utetezi, Geoffrey Mwakasege, amepinga hukumu hiyo akidai kuwa mahakama haikuzingatia ipasavyo vielelezo muhimu vilivyowasilishwa.

Alivitaja vielelezo hivyo kuwa ni pamoja na ramani ya eneo la tukio, ripoti ya uchunguzi wa DNA pamoja na maelezo ya onyo ya mshtakiwa.

Mwakasege alidai kuwa kulikuwa na mkanganyiko katika ushahidi wa kitaalamu, akieleza kuwa mtaalamu wa DNA alidai kupokea vipande vya mifupa pekee, huku baadhi ya mashahidi wakidai waliona vipande vya nyama, jambo lililoleta sintofahamu.

Aidha, alieleza kuwa maelezo ya onyo ya mshtakiwa hayakuwa na saini yake, hali iliyosababisha mahakama kutoyazingatia.

Aliongeza kuwa mahakama iliegemea zaidi katika hoja kwamba mtoto alipotea akiwa mikononi mwa mshtakiwa, jambo lililochangia kwa kiasi kikubwa hukumu hiyo.

“Mahakama yenyewe imekiri kuwepo kwa mashaka katika ushahidi wa DNA, lakini bado imetoa adhabu hiyo licha ya uwepo wa walakini,” alisema Mwakasege.

Pia alidai kuwa ushahidi uliopatikana katika shimo la choo haukuweza kuthibitishwa moja kwa moja kuwa ni wa viungo vya binadamu, jambo linaloacha maswali kuhusu msingi wa hukumu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, wakili huyo alisema upande wa utetezi haujaridhishwa na uamuzi wa mahakama, na kwamba mshtakiwa ana haki ya kukata rufaa iwapo ataona inafaa.

Kesi hiyo imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa wananchi kutokana na ukatili wa tukio hilo, huku wengi wakitoa wito kwa jamii kuachana na imani za kishirikina na kujiepusha na vitendo vya kujipatia mali kwa njia zisizo halali.

 




 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...