Skip to main content

PROF. JANABI AZINDUA WODI YA WATOTO NJITI HOSPITALI YA WILAYA YA KWIMBA, MWANZA

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Prof. Mohamed Janabi amezindua wodi ya kwanza na ya kisasa nchini kwa ajili ya watoto njiti, iliyojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.

Prof. Janabi amefanya uzinduzi huo jumamosi Februari 28, 2028 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus ambapo ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 2.125 ikijumuisha jengo, vifaa tiba na mbili nyumba za watumishi.

Prof. Janabi ametumia fursa hiyo kuipongeza taasisi ya Doris Mollel (Doris Mollel Foundation- DMF) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Keep a Child Alive (KCA) na Shirika la JHPIEGO  kwa kufanikisha mradi huo utakaosaidia kuzuia vifo vya wazazi na watoto hasa wanaozaliwa kabla ya wakati ama chini ya uzito.

"Kila mwaka Kanda ya Afrika inapoteza watoto milioni hivyo WHO tutaendelea kuunga mkono jitihada hizi ili kuhakikisha hakuna mtoto ama mzazi anapoteza maisha" amesema Prof. Janabi huku pia akiipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada inazoendelea kuchukua kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuboresha huduma za afya.

Mkurugenzi wa DMF, Doris Mollel amesema wazo la ujenzi wa wodi hiyo lilianza mwaka 2021 taasisi hiyo ilipoenesha kampeni ya kuchangia vifaa tiba kwa ajili ya wodi za watoto njiti nchini ambapo Wilaya ya Kwimba ilibainika kuwa kwenye uhitaji wa wodi na hivyo kuanza mchangato wa kutafuta fedha zilizofanikisha kukamilisha mradi huo.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la JHPIEGO Tanzania, Alice Christensen amesema kukamilika kwa wodi hiyo kutatoa mfano kote nchini namna wodi za watoto njiti zinavyopaswa kuwa hatua itakayosaidia kuokoa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua ambapo shirika hilo limechangia zaidi ya shilingi milioni 200 kwenye utekelezaji wa mradi huo.

Kwa upande wao baadhi ya wakazi wa Kwimba akiwemo Modesta Malashi, Vumilia Ally na Mariam Lucas wamesema wodi hiyo itawaondolea adha ya kubanana kwenye wodi ya pamoja iliyokuwepo awali hospitalini hapo huku pia wakilazimika kusafiri umbali mrefu hadi Bugando inapotokea changamoto ya kujifungua.
Na George Binagi, Mwanza


Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (wa tano) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto wachanga waliozaliwa kabla ya wakati (watoto njiti) katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.


Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (mwenye kofia) akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.

Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi (mwenye kofia) akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa jengo la wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza iliyojengwa na taasisi ya Doris Mollel kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la JHPIEGO na Taasisi ya Keep a Child Alive. Profesa Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Viongozi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza ambayo imegharibu shilingi bilioni 2.125 ikijumuisha jengo, vifaa na nyumba za watumishi. Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi amefanya uzinduzi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus kwenye hafla ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Naibu Waziri wa Afya, Florence Samizi akizungumza uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Elikana Balandya akizungumza kwenye hafla hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda.
Mkurugenzi Shirika la JHPIEGO Tanzania, Alice Christensen akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Mkurugenzi wa Doris Mollel Foundation (DMF), Doris Mollel akizungumza kuhusu ujenzi wa wodi ya watoto njiti katika hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza na kutoa shukurani kwa wadau wote ikiwemo Shirika la JHPIEGO kwa kusaidia ujenzi wa wodi hiyo.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika- Prof. Mohamed Janabi, Viongozi wa Serikali na wadau wa maendeleo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa wodi ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Viongozi na wadau mbalimbali wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Prof. Mohamed Janabi akimpongeza mmoja wa akina mama katika wodi mpya ya watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Baadhi ya wazazi katika wodi ya watoto njiti iliyopo Hospitali ya Wilaya Kwimba mkoani Mwanza wakifurahia mazungumzo na viongozi wakati wa uzinduzi wa wodi hiyo.
Mwonekano wa miongoni mwa nyumba za watumishi zilizojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.
Kikundi cha Sungusungu Wilaya ya Kwimba kikitoa burudani ya asili wakati wa uzinduzi wa wodi ya watoto njiti iliyojengwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba mkoani Mwanza.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...