Skip to main content

Ugonjwa wa Mapele Ngozi kwa Ng’ombe Kupatiwa Ufumbuzi

Daktari wa Mifugo Mfawidhi wa ZVC Iringa, Dkt. Jeremia Choga (L) wakati wa zoezi la uchukuaji sampuli. 

Na Friday Simbaya, Iringa

 

Ugonjwa wa Mapele Ngozi (Lumpy Skin Disease - LSD) umeendelea kuwa miongoni mwa magonjwa hatari yanayoathiri mifugo, hususan ng’ombe, na kusababisha hasara kubwa kwa wafugaji kutokana na gharama za matibabu na vifo vya wanyama.

 

Hivi karibuni, ugonjwa huo umeripotiwa kushambulia maeneo ya Nyanda za Juu Kusini, hasa katika Halmashauri ya Wilaya ya Momba mkoani Songwe, hali iliyosababisha taharuki kwa wafugaji. Takwimu zinaonesha kuwa takribani ng’ombe 750 wameathirika na baadhi kufa katika kipindi cha Februari hadi Machi, 2026 wilayani humo.

 

Kufuatia mlipuko huo, Serikali kupitia wataalamu kutoka Kituo cha Huduma za Mifugo Nyanda za Juu Kusini (ZVC Iringa) na Taasisi ya Chanjo za Mifugo Tanzania (TVI), wameweka kambi wilayani Momba kwa ajili ya kufuatilia hali ya ugonjwa huo na kuchukua sampuli kutoka kwa wanyama walioathirika.

 

Lengo la zoezi hilo ni kufanya uchunguzi wa kisayansi maabara utakaosaidia kubaini chanzo cha ugonjwa na hatimaye kuzalisha chanjo ya kudhibiti na kuzuia maambukizi yake.



Akizungumza wakati wa zoezi la uchukuaji sampuli, Daktari wa Mifugo Mfawidhi wa ZVC Iringa, Dkt. Jeremia Choga, alisema serikali inaendelea kuwajali wafugaji kwa kuhakikisha wanapata huduma bora za mifugo ili kuongeza tija katika ufugaji.

 

“Serikali inatambua umuhimu wa sekta ya mifugo katika uchumi wa nchi. Ndiyo maana imekuwa ikichukua hatua mbalimbali, ikiwemo ujenzi wa majosho, utoaji wa dawa za kuogeshea mifugo pamoja na chanjo ya ugonjwa wa homa ya mapafu ya ng’ombe (CBPP) kwa gharama nafuu,” alisema Dkt. Choga.

 

Aliongeza kuwa serikali imejipanga kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa na hatimaye kupatiwa ufumbuzi wa kudumu.

 Kwa upande wake, mtafiti kutoka Taasisi ya Chanjo za Mifugo Tanzania (TVI), Dkt. Fredy Makoga, alisema jukumu kuu la taasisi hiyo ni kufanya tafiti na kuzalisha chanjo mbalimbali za mifugo ili kuboresha sekta ya ufugaji nchini.

 

“Tunawahakikishia wafugaji kuwa tunaendelea na juhudi za kutafuta suluhu ya ugonjwa huu, kama tunavyofanya kwa magonjwa mengine ya mifugo kama homa ya mapafu ya ng’ombe (CBPP), chambavu (Black Quarter) na kimeta (Anthrax),” alisema.

 

Katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa huo, wafugaji wamehimizwa kuzingatia usafi wa mifugo yao, hususan kuogesha mara kwa mara ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa katika maeneo mengine.

 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...