Skip to main content

VIWANDA MKOANI PWANI VYATAKIWA KUBORESHA MAZINGIRA YA KAZI

 

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akizungumza na menejimenti ya Kiwanda cha Keds Tanzania Co. Ltd kinachozalisha bidhaa mbalimbali za usafi katika ziara ya kikazi Mkoani Pwani.

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akitembelea maeneo mbalimbali katika Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya Wilayani Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026. Alioambatana nao ni Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, Mkurugenziwa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma na Watendaji wenginekatika Ofisi ya Waziri Mkuu.
Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Watendaji wengine katika Ofisi yaWaziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano) wakifuatilia maelekezo ya Naibu Waziri waNchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo (hayupopichani), wakati wa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Rahma Kisuo, akiangalia bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha Aluminium Trailers Ltd wakatiwa ziara yake ya kikazi aliyofanya katika Wilaya ya Kibaha Mkoani Pwani Machi 2-3, 2026.


 Na Fredy Mgunda,Pwani

Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira na Mahusiano), Rahma Kisuo, ameziagiza menejimenti za viwanda Mkoani Pwani kuboresha mazingira ya kazi namaslahi ya wafanyakazi ili kuwa na uzalishaji endelevu na wenye tija.

Ametoa agizo hilo katika ziara yake ya kufuatilia utekelezaji wa sheria mbalimbali za kazi ikiwemo Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003 katikamaeneo mbalimbali ya kazi Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani.

Akizungumza kwa nyakati tofauti katika viwanda vilivyotembelewa, Naibu Waziri Kisuoamesema pamoja na viwanda hivyo kufanya kazi nzuri ya uzalishaji na kutekelezasheria za kazi, ziara yake imabaini dosari ndogo ndogo zinazopaswa kurekebishwa nawahusika.

“Tumetembelea baadhi ya maeneo katika viwanda hivi na kujionea hali ilivyo. Kimsingiwanafanya vizuri japokuwa kuna kasoro chache tulizozibaini ikiwemo baadhi yawafanyakazi kutokuwa na mikataba ya ajira pamoja na kutokidhi baadhi ya viwango vyausalama na afya mahali pa kazi,” amesema Naibu Waziri Kisuo.

Amewaagiza watendaji kutoka Ofisi yake na Mamlaka nyingine za udhibiti, kutengamuda maalum wa kufanya ukaguzi wa kina katika viwanda hivyo ili kutoa ushauri stahikiwa maboresho yanayohitajika kwa wawekezaji.

Aidha, amewapongeza wamiliki wa viwanda husika kwa uzalishaji wenye mchangomkubwa katika uchumi wa nchi kupitia kodi inayolipwa serikalini pamoja na kuzalishaajira nyingi kwa Watanzania.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, ambaye aliambatana na Naibu Waziri katika ziara hiyo, ameeleza baadhi yamapungufu yaliyobainika katika mifumo ya usalama na afya ya viwandavilivyotembelewa ikiwa ni pamoja na mazingira ya kazi yenye joto kali, vumbi la makaaya mawe kutapakaa katika mazingira, upungufu wa vifaa kinga na ukosefu wa alama za usalama.

Amemhakikishia Naibu Waziri kuwa watalaam wake watashirikiana na mamlakanyingine kufanya ukaguzi wa kina ambao utawezesha wawekezaji kupata ushauriunaohitajika ili kuboresha mazingira yao ya uzalishaji.

Kwa upande wao, viongozi wa viwanda vilivyotembelewa akiwemo Bw. Jacob Lerise, Msimamizi wa Rasilimali Watu na Utawala katika Kiwanda cha uundaji magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd, wamemshukuru Naibu Waziri na watendaji wake na kuahidikutekeleza maagizo mbalimbali yaliyotolewa katika ziara hiyo.

Ziara hiyo ya siku mbili Wilayani Kibaha Mkoani Pwani imefanyika katika kiwanda cha bidhaa za usafi cha Keds Tanzania Co. Ltd, Aluminium Trailers Ltd ambao ni waundajiwa trela za malori, kiwanda cha kuunda magari cha GF Vehicle Assemblies Ltd pamojakiwanda cha sabuni na vipodozi cha Creative Intertraders Ltd.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...