Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Kasper Mmuya, anatarajiwa kuzindua rasmi kliniki hiyo
Machi 4, 2026 katika Viwanja vya Garden Posta, Halmashauri ya Manispaa ya
Iringa.
Rai hiyo imetolewa na Kamishna
Msaidizi wa Ardhi Mkoa wa Iringa, Bi. Rehema Kilonzi, katika mahojiano maalumu
ofisini kwake. Amesema kliniki hiyo inalenga kutoa elimu, ushauri na huduma za
haraka kwa wananchi kuhusu masuala ya umiliki na usimamizi wa ardhi.
“Wananchi wafike kwa wingi katika
viwanja vya Garden Posta ili kupata huduma mbalimbali zinazotolewa, ikiwemo
elimu na ushauri wa masuala ya ardhi, utoaji wa hatimiliki papo kwa papo,
makadirio ya kodi ya pango la ardhi pamoja na uhuishaji wa miliki zilizoisha
muda wake,” alisema Kilonzi.
Kliniki hiyo iliyopewa jina la
‘Samia Ardhi Kliniki’ ilianza Machi 2 na itahitimishwa Machi 7, 2026, ikiwa ni
mpango maalumu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wa kusogeza
huduma karibu na wananchi.
Kwa upande wake, Afisa Ardhi wa
Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Bi. Catherine Charwe, alisema mwitikio wa
wananchi ni mkubwa, hasa wanawake wanaojitokeza kupata huduma na ufafanuzi wa
changamoto za umiliki wa ardhi.
Alisema ushiriki huo unaonesha
kuongezeka kwa uelewa wa wanawake kuhusu umuhimu wa kumiliki ardhi na kutambua
haki zao za kisheria.




Comments