Skip to main content

DK TULIA AWAFARIJI WAATHIRIKA WA MAPOROMOKO RUNGWE, ATOA MSAADA WA MCHELE NA FEDHA



Na Mwandishi Wetu

Mbeya. Spika wa Bunge Mstaafu, Tulia Ackson, ametoa msaada wa mchele kilo 400 pamoja na Sh4.4 milioni kwa familia 22 zilizoathirika na maafa ya maporomoko ya tope katika Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya.

Dkt Tulia, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Uyole na Rais wa Inter-Parliamentary Union (IPU), alikabidhi msaada huo Aprili 1, 2026 baada ya kutembelea na kukagua maeneo yaliyoathirika kufuatia maporomoko hayo yaliyotokea usiku wa kuamkia Machi 25, 2026, baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali.

Katika ziara hiyo, Dkt Tulia alitembelea familia zilizoathirika na kutoa msaada wa chakula pamoja na fedha kwa lengo la kuwafariji wahanga, akisema bado kuna mahitaji makubwa kwa waathirika hao.

“Tumetembelea familia katika kata za Lupepo, Kinyara, Ikuti, Kawetele na Nkunga. Hali siyo nzuri—wengi wamepoteza makazi na wanaishi kwa majirani. Wanahitaji chakula, magodoro na makazi bora. Tunawaomba wadau kujitokeza kusaidia,” amesema.

Aidha, alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kwa hatua za haraka zilizochukuliwa tangu kutokea kwa maafa hayo, pamoja na uongozi wa wilaya kwa juhudi za kukabiliana na athari za tukio hilo.

Katika hatua nyingine, Dkt Tulia alitoa wito kwa jamii na wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia familia zilizoathirika, akisisitiza umuhimu wa mshikamano katika kipindi hiki kigumu.

Mmoja wa waathirika, Joshua George, mkazi wa kata ya Kinyara aliyepoteza watoto wawili, alimshukuru Dkt Tulia kwa msaada na faraja, akisema hatua hiyo imewapa nguvu ya kuendelea na maisha licha ya changamoto kubwa wanazokabiliana nazo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Rungwe, Mekson Mwakipunga, alisema tukio hilo limeacha majonzi makubwa, huku baadhi ya familia zikibaki bila makazi baada ya nyumba zao kusombwa na maporomoko hayo.

Alieleza kuwa katika Kijiji cha Mboyo, familia moja ilipoteza watu wanne, huku mmoja wa wanafamilia akidaiwa kunywa sumu kutokana na maumivu ya kupoteza wajukuu zake watatu.

Mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...