Skip to main content

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI UJENZI WA SOKO LA MACHINGA IRINGA KUANZA



Na Friday Simbaya, Iringa

Serikali imeeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Soko la Machinga Complex katika Manispaa ya Iringa, uliopitishwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati.

Akijibu swali la Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo, bungeni, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Festo Dugange, alisema mradi huo unatarajiwa kujengwa katika eneo la zamani la stendi ya mabasi, Kata ya Kitanzini, lenye ukubwa wa mita za mraba 6,555 kwa gharama ya Sh bilioni 4.67.

Alifafanua kuwa soko hilo litakuwa na vizimba 800, maduka 150 na migahawa 8, na linatarajiwa kuhudumia wafanyabiashara 958, wakiwemo wafanyabiashara wadogo 800, wa kati 150 pamoja na mama na baba lishe 8.

Kwa mujibu wa Dugange, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetenga Sh milioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya awali ya ujenzi wa mradi huo.

Akichangia hoja, Mbunge Ngajilo aliishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wa kuanzisha mradi huo, akieleza kuwa utakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Iringa Mjini. Aidha, alihoji kama wafanyabiashara, hususan wamachinga, watahusishwa kabla ya kuanza kwa ujenzi huo na ni lini utekelezaji utaanza rasmi.

Akijibu hoja hizo, Serikali ilisisitiza kuwa ushirikishwaji wa wadau ni hatua ya msingi katika utekelezaji wa miradi yote ya kimkakati, ikiwemo kuwahusisha viongozi wa halmashauri, madiwani na wafanyabiashara wa eneo husika.

Serikali imeelekeza Manispaa ya Iringa kuandaa andiko la mradi na kuliwasilisha Tamisemi kwa ajili ya tathmini na utafutaji wa fedha za kuunga mkono utekelezaji wake. Pia imesisitiza umuhimu wa halmashauri kuendelea kutenga fedha kila mwaka kupitia mapato ya ndani.

Imeelezwa kuwa baada ya kukamilika kwa hatua za maandalizi, ujenzi wa soko hilo utaanza kwa kuzingatia maoni na mahitaji ya wafanyabiashara waliolengwa kunufaika na mradi huo.


 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...