Skip to main content

Majeruhi wa Ajali ya Shabiby na Lori Wasimulia Walivyookoka Kifo Iringa



Baadhi ya majeruhi wa ajali iliyohusisha basi la kampuni ya Shabiby na lori la mizigo lililokuwa likisafirisha vinywaji baridi aina ya Pepsi wameeleza kwa masikitiko namna walivyookoka katika tukio hilo lililotokea katika Kijiji cha Tanangozi, Kata ya Mseke, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa.

Ajali hiyo ilitokea baada ya magari hayo kugongana uso kwa uso, na kusababisha vifo na majeraha kwa abiria kadhaa.

Mwandishi wa The Guardian alitembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa na kuzungumza na baadhi ya majeruhi wanaoendelea kupatiwa matibabu, huku wengine wengi wakiwa tayari wameruhusiwa baada ya hali zao kuimarika.

Mmoja wa majeruhi hao, Juma Shaban, mwalimu wa Songwe Tech Secondary School mkoani Songwe, alisema wakati ajali inatokea alikuwa amelala usingizi ndani ya basi akiwa safarini kuelekea Mbeya.

“Nilikuwa nimelala kabisa. Ghafla nikasikia kelele za watu wakivunja vioo vya basi ili kuwaokoa abiria. Nilipojitambua nilikuwa navuja damu nyingi na mguu wangu ulikuwa umevunjika,” alisema Juma akiwa wodini.

Majeruhi mwingine, Elias Mwakilomo, mkazi wa Tarime na mhasibu wa Mgodi wa Nyamongo, alisema alikuwa akisafiri kwenda Mbeya kuhudhuria msiba wa bibi yake.

“Nilishtuka tu nikijikuta mbavu zangu zimebanwa kwenye siti. Wananchi wa eneo lile walinisaidia kunitoa, lakini sikuweza kuokoa kitu chochote,” alisema.

Mwakilomo alisema katika ajali hiyo alipoteza simu yake pamoja na kompyuta mpakato aina ya MacBook Air. Madaktari walimfanyia upasuaji mdogo wa kuondoa damu na usaha kwenye kifua, na hali yake inaendelea vizuri.

Naye Ben Lilawola, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Iringa (UoI), ambaye aliumia jicho la kulia, alisema aliona lori likifanya overtake katika kona kwa mwendo mkubwa kabla ya kuligonga basi walilokuwa wakisafiria.

“Niliona lori likiovertake ghafla. Sekunde chache baadaye likagonga basi letu. Baada ya hapo nikahisi kitu kizito kimenibana kichwani,” alisema Ben, ambaye anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa jicho.

Wakati huo huo, ndugu wa raia wa India aliyefariki dunia katika ajali hiyo wameeleza masikitiko yao kufuatia kifo hicho.

Mmoja wa ndugu hao, Zain Mukadam maarufu kama Kaza Roho, alisema walifika hospitalini kwa ajili ya kumtambua ndugu yao, Tejas Jaral (31), lakini baadaye walielezwa kuwa alikuwa amefariki dunia majira ya saa moja usiku.

Alisema marehemu alikuwa akisafiri kutoka Dodoma kwenda Mbeya kwa shughuli za kikazi, huku akiishi na kufanya kazi jijini Dar es Salaam.

“Tumeanza mawasiliano na ubalozi kuhusu taratibu za kusafirisha mwili kwenda India kwa ajili ya mazishi, kwani hapa Tanzania hakuwa na ndugu wa karibu,” alisema.

Mukadam aliwashauri wasafiri kuhakikisha wanaandika majina yao sahihi pamoja na namba za simu za ndugu wa karibu ili kurahisisha utambuzi na mawasiliano wakati wa dharura.

Pia alitoa wito kwa Jeshi la Polisi na kampuni za usafiri kuhakikisha magari ya abiria yanakuwa na orodha kamili ya wasafiri ili kurahisisha utambuzi wa waathirika endapo ajali zitatokea.


Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Dk Alfred Mwakalebela, alisema hali za majeruhi wengi zinaendelea vizuri, huku wagonjwa watatu pekee wakiendelea kulazwa hospitalini.

“Kwa sasa wagonjwa watatu wanaendelea kupatiwa matibabu. Hali zao zinaendelea vizuri na tunawafuatilia kwa karibu,” alisema Dk Mwakalebela.

Ajali hiyo imeacha majonzi makubwa kwa familia za waliopoteza ndugu zao na kuibua tena mjadala kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria za usalama barabarani ili kuokoa maisha ya Watanzania.

Mwisho


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...